Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ametangaza vita na Wafanyabiashara wanaouza Sukari kwa bei ghali tofauti na bei elekezi ya Serikali ambapo amesema ifikapo Kesho kikosi kazi kitafanya ukaguzi na watakaobainika kuuza bidhaa hiyo kwa bei ya juu Watakamatwa na Sukari kutaifishwa na Serikali.
RC Makonda amewaelekeza Wakuu wa Wilaya zote Tano za Mkoa huo kuhakikisha msako huo unaanza kesho na asisalie Mfanyabiashara yoyote anaeuza Sukari hiyo kwa Bei ya Juu.
Hatua hiyo imekuja baada ya RC Makonda kubaini uwepo wa baadhi ya wafanyabiashara wanaouza Sukari kwa bei ya hadi Tsh 4,500 kinyume na bei elekezi ya serikali ya Tsh 2,600 jambo linalopelekea maumivu na gharama kwa wananchi.
RC Makonda amewaelekeza Wakuu wa Wilaya zote Tano za Mkoa huo kuhakikisha msako huo unaanza kesho na asisalie Mfanyabiashara yoyote anaeuza Sukari hiyo kwa Bei ya Juu.
Hatua hiyo imekuja baada ya RC Makonda kubaini uwepo wa baadhi ya wafanyabiashara wanaouza Sukari kwa bei ya hadi Tsh 4,500 kinyume na bei elekezi ya serikali ya Tsh 2,600 jambo linalopelekea maumivu na gharama kwa wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...