Na Khadija Seif, Michuzi TV.

MSANII anayekimbiza kwenye tasnia ya uchekeshaji nchini, Abdallah Sultan a.k.a Dullivan amezindua rasmi shindano la "Asante fans".

Dullivan amesema kuwa kutokana na kupokelewa kwake vizuri na mashabiki zake ameamua kurudisha fadhila kwa mashabiki zake kupitia shindano hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari amesema kuwa vigezo vya kushiriki kwenye shindano hilo ni kumfwatilia kwenye mitandao yake ya kijamii kwa njia ya kuchangia ujumbe mfupi na  kuwa-tag watu wa tano kwenye picha ambazo atakuwa anatuma kwenye mtandao wake wa Instagram na kupata mshindi.

"Shindano hilo litakuwa  kwa kila wiki kwa njia ya simu na hii nimeamuwa kufanya hivyo kwa lengo la kurudisha asante kwa mashabiki zangu kwa mafanikio ambayo nimepata tangu nimeanza kazi zangu za uchekeshaji"

Aliongezea kuwa kwa wiki hii mshindi atapata kiasi cha fedha laki 5 kwa watu wa tano na kwamba shindano hilo halichagui ni kwa watu wote.

Hata hivyo Dullivan ameeleza kuwa jamii inayomzunguka bado inaendelea kumpa nguvu hasa mama yake mzazi tangu ameanza kazi hiyo mpaka Sasa hivyo hategemei kukatishwa tamaa kutokana na kuvaa uhusika wa kike (mama chogo) kuanzia mavazi,lafudhi pamoja na madoido .

''Wakati mwingine mama yangu mzazi mwenyewe ananichagulia mavazi Kama vijora na ananishauri kabisa vitanipendeza kutokana na rangi zake hivyo naona ndio baraka ananimwagia na anachukulia Kama kazi zingine tu ndio maana nafanikiwa napata kazi nyingi na ndio maana napata na mimi nguvu ya kurudisha fadhila kwa mashabiki,".

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...