TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imefanikisha kurejesha jengo la mjane Jane Duncan Kaaya ambalo liliporwa na ofisa maendeleo ya jamii wa kata ya Kibaya, Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, Janeth Paulo na kutumiwa kukodishwa kama ghala la kuhifadhi mazao. 

Akizungumza jana Mkuu wa TAKUKURU, Mkoani Manyara, Holle Joseph Makungu akizungumza alisema mjane huyo aliporwa jengo hilo na ofisa huyo wa maendeleo ya jamii wa Kata ya Kibaya Janeth Paulo tangu mwaka 2017 hadi lililoporudishwa Mei 21. 

Makungu alisema mjane huyo aliporwa jengo hilo baada ya mume wake marehemu Duncan Kaaya kukopa fedha kwenye taasisi moja ya fedha mwaka 2016 na kushindwa kurejesha hadi akafariki.

Alisema baada ya hali hiyo taasisi hiyo ya fedha iliuza jengo hilo kwa ofisa maendeleo huyo wa jamii Janeth kwa shilingi milioni 35. 

Alisema hata hivyo kutokana na changamoto za kisheria Janeth alishindwa kumilikishwa hivyo akaishtaki taasisi hiyo na akarejeshewa fedha zake ila hakurudisha jengo hilo. 

Alisema uchunguzi wao umebaini kuwa Janeth alirejeshewa fedha zake na shilingi milioni 3 za usumbufu ila akaendelea kudai kuwa ni mali yake akajimilikisha. 

"Pia pamoja na kurejeshewa fedha zake ofisa maendeleo huyo tangu mwaka 2017 aliendelea kuchuma fedha na kujipatia kipato bila uhalali hadi uchunguzi wa Takukuru ulipoanzishwa," alisema Makungu. 

Alisema pamoja na kumrejeshea Kaaya jengo hilo hatua kali zitachukuliwa dhidi ya ofisa maendeleo huyo asiye na chembe ya huruma kwa wajane ambaye amekuwa akijipatia fedha kwa njia ya udanganyifu. 

Aliwahimiza watanzania kuendelea kutoa taarifa za vitendo vya rushwa, ufisadi na dhuluma kwenye jamii kupitia namba yao ya dharura ya 113 au kufika kwenye ofisi zao za mkoa na wilaya na wakipata taarifa wanazifanyia kazi kwa misingi ya kisheria. 
 Mjane Jane Duncan Kaaya mkazi wa Kata ya Kibaya Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, (katikati) akipatiwa nyaraka ili atie saini baada ya TAKUKURU kumsaidia kupata jengo lake lililoporwa na ofisa maendeleo ya wjamii wa Kata hiyo hivyo kurejeshewa, anayeshuhudia kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo mhandisi Tumaini Magessa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...