Na Karama Kenyunko,Michuzi TV
MAHAKAMA ya Hakimu Kisutu imewahukumu wafanyabiashara wanne wakazi wa Dar es Salaam kulipa faini ya shilingi 500,000 kila mmoja ama kifungo cha miaka mitatu jela kwa kosa la kukutwa na madini tofauti tofauti yenye uzito gram 131 yenye thamani ya zaidi shilingi milioni 100 kinyume na sheria.
Wafanyabiashara hao Noah Mmasanga, Richard Boniface, Ally Said na Mosses Mbojo ambapo wamehukumiwa kulipa faini hiyo baada ya kufika makubaliano na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini DPP ya kukiri makosa yaliyokuwa yakiwakabili.
Hukumu hiyo imesomwa leo mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Mwandamizi Vicky Mwaikambo baada ya kujiridhisha na vielelezo vilivyo wasilishwa mahakamani hapo na upande wa Mashtaka ukiongozwa na wakili wa serikali mwandamizi Renatus Mkude.
Akiwasilisha hoja ya upande wa Jamuhuri Wakili Rwnatus Mkude alidai vielelezo vilivyokamatwa ni pamoja na Madini aina ya Tanzanite, Ruby, Vocanic Glass gram 131 pamoja na kadi ya gari aina ya Toyota Raum yenye namba za usajili T 716 DJP.
Baada ya Mahakama kujiridhisha na vielelezo hivyo, Wakili Mkude akaiomba mahakama hiyo kutaifisha madini hayo pamoja na gari lililotumika kusafirisha madini hayo nakulipa faini kama walivyofikia makubaliano na DPP.
Hata hivyo baada ya kusikiliza hoja za pande zote, Hakimu Mwandamizi Mwaikambo aliamuru nyara hizo kutaifishwa kuwa Mali ya serikali nakuwataka washitakiwa kulipa faini kwa mujibu wa sheria ama kifungo cha miaka mitatu jela.
Washtakiwa hao hakuwa na pingamizi yoyote juu ya maamuzi hayo baada ya mahakama kuwatia hatiani na kukiri kosa.
MAHAKAMA ya Hakimu Kisutu imewahukumu wafanyabiashara wanne wakazi wa Dar es Salaam kulipa faini ya shilingi 500,000 kila mmoja ama kifungo cha miaka mitatu jela kwa kosa la kukutwa na madini tofauti tofauti yenye uzito gram 131 yenye thamani ya zaidi shilingi milioni 100 kinyume na sheria.
Wafanyabiashara hao Noah Mmasanga, Richard Boniface, Ally Said na Mosses Mbojo ambapo wamehukumiwa kulipa faini hiyo baada ya kufika makubaliano na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini DPP ya kukiri makosa yaliyokuwa yakiwakabili.
Hukumu hiyo imesomwa leo mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Mwandamizi Vicky Mwaikambo baada ya kujiridhisha na vielelezo vilivyo wasilishwa mahakamani hapo na upande wa Mashtaka ukiongozwa na wakili wa serikali mwandamizi Renatus Mkude.
Akiwasilisha hoja ya upande wa Jamuhuri Wakili Rwnatus Mkude alidai vielelezo vilivyokamatwa ni pamoja na Madini aina ya Tanzanite, Ruby, Vocanic Glass gram 131 pamoja na kadi ya gari aina ya Toyota Raum yenye namba za usajili T 716 DJP.
Baada ya Mahakama kujiridhisha na vielelezo hivyo, Wakili Mkude akaiomba mahakama hiyo kutaifisha madini hayo pamoja na gari lililotumika kusafirisha madini hayo nakulipa faini kama walivyofikia makubaliano na DPP.
Hata hivyo baada ya kusikiliza hoja za pande zote, Hakimu Mwandamizi Mwaikambo aliamuru nyara hizo kutaifishwa kuwa Mali ya serikali nakuwataka washitakiwa kulipa faini kwa mujibu wa sheria ama kifungo cha miaka mitatu jela.
Washtakiwa hao hakuwa na pingamizi yoyote juu ya maamuzi hayo baada ya mahakama kuwatia hatiani na kukiri kosa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...