NaFarida Saidy,Morogoro.

Kufuatia athari zilizojitokeza za mafuriko kwa baadhi ya vijiji vya wilaya ya kilombero mkoani Morogoro baada ya maji kufunguliwa katika bwawa la kufua umeme la Kidatu mawaziri wawili wa Nishati Dkt.Medard Kalemani na Mussa Zungu wa Muungano na Mazingira wamefanya ziara ya kukagua madhara yaliyojitokeza katika Wilaya hiyo.

Lengo la ziara hiyo ni kunagalia namna ya kudhibiti uharibufu uliojitokeza katika mabwawa ya kuzalishia umeme ya Mtera na Kidatu,ambapo Waziri wa Nishati Mhe Medard Kalemani amewataka wananchi wanaofanya shughuri za kibinaadamu pembezoni mwa mto Ruaha mkuu kuacha mala moja kwani wanaharibu mazingira.

Hata hivyo Waziri kelemani amesema wao Kama wizara ya Nishati wanawajibu wa kulinda na kutunza miundombinu yote ya uzalishaji wa umeme, hivyo wanashirikiana na Nemc na wadau wengine wa mazingira ili kuulinda mradi mkubwa wa bwawa la kufua umeme la Julius NyerereMW 2115,kwani maji yanayotoka katika mto Ruaha Mkuu ndioyanayoenda katika mradi huo mkubwa wa kufua umeme wa Julius NyerereMW 2115.

Kwa upande wake Waziri wa Muungano na Mazingira Mhe Mussa Zungu amewataka Nemc kwa kushirikiana na wadau wote wanaohusika na Mazingira kukutana ndani ya sikuku kumi ili kutoa tathmini ya uharibifu uliotokea katika kipindi ambacho maji yamefunguliwa katika mabwawa ya Mtera na Kidatu.

Hata hivyo kwasasa maji yamepungua katika mto Ruaha Mkuu ukilinganisha na kipindi cha nyuma ambapo maji hayo yalitishia hata uhai wa daraja la mto huo linalotenganisha wilaya mbili za Kilosa na Kilombero

Aidha mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare anabainisha namna ambavyo wananchi wake waliathirika huku wengine wakikosa makazi ya kwa sababu ya maji kujaa kwenye maeneo yao, huku mwenyekiti wa bodi ya baraza la taifa ya mazingira akibainisha moja ya kisababishi cha athari zilizojitokeza Ni wananchi kufanya shughuri za kibinaadamu ikiwemo Kilimo kwenye kingo za mto huo.

Kujaa kwa mabwawa ya kufua umeme hapa nchini ni kiashiria cha uwepo wa umeme wa uhakika kwa matumizi mbalimbali ya kiuchumi.
Waziri wa Nishati Mhe Medard Kalemani akizungumza na Waandishi wa habari hawapo picha,alipofanya ziara ya kukagua athari zilizotokana na  mvua iliyosababisha kufunguliwa kwa maji katika bwawa la kuzalishia  umeme kidatu Wilayani kilombero, kulia Ni Waziri wa Muungano na Mazingira Mhe Mussa Zungu aliyeambatana naye kujionea athari hizo.
 Waziri wa Muungano na Mazingira Mhe Mussa Zungu akitoa maelekezo kwa timu ya watalaam wa Nemc waliofika kujionea athari za mvua katika mto Ruaha Mkuu unaotenganisha Wilaya ya kilombero na Kirosa Mkoani Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...