NMB Madaraka
NMB Bank House
NMB Kenyatta
NMB Clock Tower



Meneja Uhusiano Mwandamizi wa NMB Kanda ya Kaskazini anayeshughulikia Kilimo- Oscar Rwechungura alisema katika kuadhimisha Wiki ya Maziwa kwa kushirikiana na wadau wengine katika sekta ya maziwa wanawezesha sekta hiyo katika mnyororo wa thamani.

“NMB inawezesha sekta hii kuanzia ngazi ya mwanzo kwa wafugaji wenyewe, wafanyabiashara wa dawa za mifugo na wasindikaji wa mazao ya maziwa katika kuhakikisha tunaimarisha sekta nzima ya maziwa na kuimarisha afya za watumiaji wakiwemo wafanyakazi wa NMB,” alisema Rwechungura

Alisema lengo la NMB ni kupanua wigo kwa wafugaji wadogo ili waweze kupata huduma za kifedha kwa njia rahisi ili kuongeza idadi ya ng’ombe, vyakula vya mifugo na huduma za matibabu ya mifugo ili kuongeza tija ya ufugaji wao.

“Lengo letu ni kuwawezesha wazalishaji wa maziwa kuongeza tija,badala ya mfugaji kutegemea kupata maziwa lita mbili kwa siku jambo ambalo halimfanyi aone faida ya kazi anayoifanya tunatamani apate lita 20 na zaidi kwa siku hivyo ili mfugaji apate faida lazima aongeze matumizi kwa kupata uwezeshwaji kutoka kwetu,”

NMB haishii kuwawezesha wafugaji wadogo na kati kupata mitaji pekee bali inawaunganisha na masoko ili kuwezesha mnyororo wa thamani katika sekta nzima ya maziwa kuanzia kwa mfugaji hadi anayepeleka maziwa sokoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...