Na.Ashura Mohamed -Arusha

Halmashauri ya Jiji la Arusha imekabidhidi Hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 626,kwa vikundi 100 vya Mikopo kwa makundi matatu ya Wanawake,Vijana na watu wenye Walemavu.

Akikabidhi Hundi hiyo Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro alisema fedha hizo ni kutoka Mapato ya ndani ambapo lengo ni kuwawezesha wananchi, kiuchumi ili kutimiza Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano.


Daqqaro alisema kuwa serikali ya Sasa imekuwa ikisisitiza uwekezaji kwenye sekta ya Viwanda hivyo aliwataka maafisa Maendeleo Kata kuhakikisha kuwa wanatumia elimu yao vizuri kuvilea vikundi ndani ya kata zao na kuviwezesha kuanzisha viwanda vidogo vidogo.

"Kwanza niwapongeze kwa kuhakikisha vikundi hivi vinapatiwa mikopo lakini pia tunataka mikopo hii ionekane kwa vitendo yaani tuone viwanda vidogo vidogo katika kata tunaajua nyie mmesoma Sana sasa tumieni elimu yenu kuwasaidia hawa wananchi kubuni viwanda vidogo vidogo na biashara zinazoonekana.

Aidha alisema kuwa sheria Kali zitachukuliwa kwa vikundi vitakavyoshindwa kurejesha vizuri mikopo hiyo huku akivitaka vikundi hivyo kuhakikisha kuwa wanapelekea fedha hizo kwenye miradi na sio matumizi mengine yasiyotarajiwa."alisema Daqqaro

"Mikopo hii zamani watu walikuwa hawazipati lakini kutokana na Rais John magufuli kusema asilimia hii ipelekwe kwa watu wake ndio maana halmashuri zinatenga na kuwapa wahusika hao,"alisema Daqqaro

Pia aliwataka Maofisa Maendeleo Kata kusimamia vizuri vikundi hivyo pamoja na kuelekeza aina za biashara za kufanya amabazo zitawazalishia fedha badala ya kuvitelekeza.

Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Mwanamsiu Dossi, alisema fedha hizo zimetokana na urejeshaji wa zaidi ya Sh.milioni 122.2 wa vikundi vilivyokopeshwa na zaidi ya Sh.milioni 504.6 zimetokana na fedha za mapato ya ndani.


Alisema mikopo hiyo iliyotolewa zaidi ya Sh.milioni 626.8 kati ya hizo Sh.milioni 377 zimetolewa kwa vikundi 65 vya wanawake,Sh.milioni 234.866 vikundi 32 vya vijana na Sh.milioni 15 vikundi vitatu vya watu wenye ulemavu.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Halmashuri ya Jiji la Arusha Dk.Maulid Madeni amemwomba Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro kuongeza kiwango cha fedha za kukopesha kwa walengwa hao ili ziwasaidie kufanya biashara.

"Sio lazima tuwapatie fedha tunaweza kuboresha mikopo hii kwa kununua mfano mashine za kufyatua matofali,ili kusaidia Vikundi vya vijana lakini pia tunaweza kuwapatia mashine za kushonea nguo wanawake Hawa wakaweza kujiajiri na pia kuweza kuzalisha na kupata faida zaidi,ili tuweze kusaidia jamii zetu vizuri.alisema Madeni

Jumla ya Vikundi 109 viliomba mikopo hiyo ambapo Vikundi 100,Vimepatiwa mikopo na Tisa vimekosa sifa huku ikiwa ni utekelezaji wa Agizo la Serikali la kutenga Asilimia kumi ya Mapato ili kuwasaidia Vijana,Wanawake na Watu wenye Ulemavu.
 Mmoja wa Vijana ambaye Ni mwakilishi wa kundi Hilo akiwa na Baadhi ya Viongozi wa jiji la Arusha katika hafla ya kupokea hundi za Mikopo.

 Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini Gabriel Daqqaro akizungumza na Vikundi vya Mikopo  ambavyo havipo Pichani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...