Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Mkuu wa Mkoa wa Mara ameipongeza Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kupata hati safi kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017.

Akizungumza hivi karibuni wakati wa uwasilishaji wa hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Selikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019, Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima aliipongeza Halmashauri ya Mji wa Bunda kwa kupata hati safi kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017, 2017/2018 na 2018/2019.

“Halmashauri hii ni ya mfano katika mkoa wa Mara na ninawaomba msibweteke kwa vile mmepata mafanikio haya, bali muongeze bidii” alisema mkuu wa mkoa Malima

Aidha, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali katika mkoa wa Mara, Patrick Lugisi alisema kuwa mafanikio hayo ni matokeo mazuri ya kazi wanayofanya watumishi wa Halmashauri ya mji wa Bunda.

“Ushirikiano na uwajibikaji wa Menejimenti ndio umepelekea Halmashauri hii kuwa na hoja chache na kuwa na ufanisi, niziombe Halmashauri zingine kuiga mfano huu” alisema Lugisi.

Halmashauri ya mji wa Bunda ilianzishwa Mwaka 2015 na ilianza kutekeleza majukumu yake Mwaka 2016. Hati safi kwa halmashauri hii imekuwa chachu ya kuongeza tija kwa watendaji wote na hivyo kuwawezesha wananchi kunufaika na huduma bora zinazotolewa katika sekta za afya, elimu, maji,miundombinu na uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...