Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Abel Makubi akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa mkataba wa huduma kwa Wateja wa TMDA kuzinduliwa katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Abel Makubi katikati akionesha mkataba wa huduma kwa wateja wa TMD kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi Erick Shitindi na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMDA Adam Fimbo.

 Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Abel Makubi akizungumza wakati wa uzinduzi mkataba wa huduma kwa Wateja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba  (TMDA) katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Adam Fimbo akitoa maelezo ya mkataba wa Huduma kwa Wateja wa Mamlaka hiyo katika Hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

======  =======  ======  =======

*Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya watakiwa kuwa na mkataba wa huduma kwa wateja.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jami, Jinsia, Wazee na Watoto imesema   Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo  zinapaswa kuwa na mkataba wa huduma kwa  Wateja  ili kurahisisha utoaji wa huduma boara  kwa wanannchi.

Hayo ameyasema  Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Abel Makubi jijini Dar es Salaam wakati akizindua mkataba wa huduma kwa wateja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), amesema kuwa TMDA imekuwa na mipango mizuri katika utoaji wa  huduma kwa kuzingatia muda katika utoaji wa leseni kwa wadau mbalimbali.

Profesa Makubi amesema kuwa TMDA imekuwa na mifumo ya viwango ambapo Shirika la Afya Duniani inatambua pamoja na jumuiya  mbalimbali na hiyo inatokana na mikakati ya watendaji wa taasisi waliojiwekea ya kuhakikisha wanakwenda kutatua matatizo ya  huduma katika utoaji wa huduma.

Amesema  kuwa TMDA inatoa mkataba  mara ya nne ambapo amewataka mamlaka hiyo  kufuatilia mkataba huo kuona malengo waliojiwekea yameweza kama wameweza waliojipangia pamoja na huduma wanazozitoa kwa wadau.

Nae Kaimu Mkurgenzi Mkuu wa TMDA Adam Fimbo amesema kuwa katika mkataba huo wamezingatia muda wa utoaji wa usajili  za waingizaji dawa kutoka siku 240 hadi 180 na wa ndani kutoka siku 120 hadi siku 60 na usajili dawa sehemu za biashara kutoka siku 10 hadi 8.

Fimbo amesema kuwa mkataba huo umezinagatia  maoni ya wadau mbalimbali ili kukidhi mahitaji ya utoaji wa huduma  na kuleta ufanisi pamoja na kuweka mikakati kuendelea kutoa huduma  bora
kwa wadau amesema  TMDA  tangu walipoanza kutengeneza mkataba wa huduma kwa wateja wamekuwa na mafanikio  makubwa  katika utoaji wa huduma bora kutokana na watendaji kujipanga katika kuhudumia wateja hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...