MSANII nyota wa miondoko ya Afro Pop, Pop na RnB kutoka Nchini Nigeria, Adefemi Ebenezer maarufu kama Olakira   Ijumaa ya 26 Juni anatarajia rasmi kuachia wimbo mpya wa ‘In my Maserati’.
 
Olakira anayetamba na nyimbo bora mbalimbali zikiwemo  ‘Aya Mi’,  ‘Wakanda Jollof na zingine nyingi ambapo kwa sasa anakuja ba ujio mpya wa wimbo wake utakaokuwa kwa sauti na video ‘In my Maserati’.
 
“Wimbo wa In my Maserati unaelezea namna anavyovutiwa na gari la kifahari aina ya Maserati akimuahidi mpenzi wake na kuliendesha gari hilo”
Wimbo huo umetayarishwa na Olakira mwenyewe huku video ikiwa imechukuliwa viunga vya Jiji la Lagos na kuongozwa na Clarence Peters.
 
Aidha, Msanii Olakira amekuwa akifanya vizuri kwenye tasnia ya muziki Nchini Nigeria na Afrika kwa ujumla kwa kutoa muziki mzuri wa Afropop.
Ujio wake katika Afropop alianza na wimbo wa  ‘Hey Lover’  na baadae wimbo wa ‘Flirty signal’ ambapo zilipokewa vizuri na kupata watazamaji (views) wengi kupitia mtandao  wa Youtube.
 
Olakira pia ameshiriki kuandika na kuandaa wimbo uliofanya vyema katika Afro wa ‘Akube’ na ‘My Woman’ wa Dotman na kumuweka katika chat za juu kwenye ramani ya muziki Afrika.
Pia mbali na kuwa ni Mwanamuziki, Olakira ni Mtayarishaji wa muziki (Producer ),mwandishi wa mashahiri ya muziki (songwriter ).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...