Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha Amina Mollel (CCM) amelieleza Bunge kuwa Rais Dkt.John Magufuli ni zawadi tuliyopewa na Mungu, hivyo kikubwa ni kuendelea kumuombea awe na maisha marefu zaidi.

Mollel amesema hayo wakati wa vikao vya Bunge vinavyoendelea Bungeni Mjini Dodoma ambapo wabunge walipata nafasi ya kujadili maazimio mawili, Azimio la kwanza ni kumpongeza Rais Magufuli na azimio la pili ni kumpongeza Spika wa Bunge Job Ndugai.

Akieleza zaidi mbele ya wabunge Mbunge Mollel amesema kuwa mara kadhaa amekuwa akitamka hapo bungeni kuwa Rais Magufuli ni zawadi ya watanzana kutoka kwa Mungu.

"Ni zawadi kwasababu ni Rais mwenye ujasiri, uthubutu, muongoza njia ambaye amekua akituongoza kuelekea uchumi wa kati.Tunajivunia kuwa na Rais Magufuli, tunajivunia kuwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, tunajivunia kuwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, tunajivunia kuwa na Baraza la Mawaziri ambalo limekuwa likimsaidia Rais kwa ukaribu zaidi katika kulipeleka taifa katika maendeleo.

"Katika mafanikio makubwa ambayo Rais Magufuli ameyafanya ni kutokana na uwepo wa wasaidizi wake ambao nao naomba niwapongeze. Nakumbuka tumekuwa tukisikia Serikali kuhamia Dodoma lakini sasa tunashuhudia chini ya Rais Magufuli Serikali imeshahamia Dodoma.

"Baada ya kupitishwa azimio hili ambalo tunalijadili hapa naamini hakutakuwa na mtu mwenye maono mengine ya kuiondoa Serikali hapa Dodoma. Haya ni maajabu ambayo yanafanywa na Rais Magufuli, amekuwa Rais wa mfano na Dodoma ambayo inaonekana leo hii baada ya miaka 10 ijayo itakuwa tofauti kabisa na hata wale ambao waliondoka hapo nyuma wakirudi leo watashangaa,"amesema Mollel.

Ameongeza kikubwa ambacho Watanzania wanatakiwa kukifanya ni kuendelea kumuombea kwa Mwenyezi Mungu Rais Magufuli ili azidi kuwa na afya njema na maisha marefu zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...