Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya leo (08.06.2020) amefanya ziara ya kushtukiza kwenye eneo la ujenzi wa vihenge vya kisasa (silos) mjini Shinyanga na kuelezea kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo .

" Mkandarasi sijaridhishwa na kazi yako kuwa na kasi ndogo wakati serikali inahitaji mradi huu wa maghala ukamilike kwa wakati.Nataka uongeze idadi ya vibarua na mafundi ili spidi ya kazi iongezeke " alisema Kusaya

Katibu Mkuu huyo ameelekeza mkandarasi kuwa ataendelea kutembelea ujenzi wa vihenge hivyo mara kwa mara bila taarifa kukagua kwani Wizara inataka   kuona vihenge na maghala hayo yanakamilika kwa wakati kwa ajili ya kuhifadhi mazao ya chakula kwa matumizi ya Taifa.

Kusaya alibainisha kuwa serikali inatekeleza mradi  huo mkubwa wa shilingi Bilioni 15.24 wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi kwa kujenga vihenge (silos) sita zenye uwezo wa kuhifadhi tani 20,000 na ghala moja kubwa lenye uwezo wa kuhifadhi tani 10,000 za nafaka katika eneo la Ibadakuli mkoani Shinyanga.

Katibu Mkuu Kusaya alikuwa njiani kutoka Mwanza kuelekea Dodoma aliposimama mkoani Shinyanga kukagua mradi huo wa ujenzi wa vihenge .
 

 
 Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (aliyevaa t-shirt mistari nya blu) akikagua eneo la ujenzi wa vihenge vya kisasa eneo Ibadakuli Shinyanga.Katibu Mkuu huyo ameeleza kutoridhishwa na kasi ya ujenzi na kutaka mkandarasi aongeze spidi.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...