Yassir Simba, Michuzi Tv
Sakata la mchezaji wa Young Africans raia wa Ghana,Bernard Morrison limechukua sura mpya ambapo kupitia nakala iliyotolewa na kaimu katibu mkuu wa klabu ya Yanga Wakili Simon Patrick leo tarehe 24/06/2020  klabu ya Yanga imeamua kumkata kiasi cha shillingi 1,500,000 pesa taslimu ya kitanzania  mchezaji huyo kutokana na kile kinachdaiwa na klabu hiyo kuwa mchezaji huyo alifanya mahojiano na chombo cha habari bila kufuata utaratibu uliowekwa na kabu.

Katika siku hizi za hivi karibuni kumekuwa na malalamiko juu ya mkataba ya mchezaji huyo kwa kile kinachodaiwa kuwa kuna baadhi ya timu zinatajwa kumnyemelea mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27,ikumbukwe Yanga na Morrison waliingia mkataba wa miezi saba na mchezaji huyo kuanzia tarehe 15/01/2020  mpaka 14/07/2020 kwa kuwa na makubaliano na mchezaji kuwa endapo klabu itaridhisha na kiwango chake mkataba utaongezwa ambapo mara baada ya Yanga kuridhishwa na kiwango chake tarehe 20/03/2020 klabu hiyo ya Yanga iliingia mkataba na Morrison kwa kuzingatia maslahi binafsi ya mchezaji huyo ambapo mkataba huo uliotakiwa kumalizika 14/07/2022 .
Mara baada ya Yanga kumuongeza mkataba mchezaji huyo, klabu hiyo iliusajili mkataba huo kwenye mifumo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na shirikisho la Mpira wa MIguu Duniani ( FIFA)
Katika siku za nyuma Morisson aliwahi kugomea kujiunga na timu katika michezo ya ligi kuu ya Tanzania bara ikiwemo mchezo wa Yanga dhidi Mwadui pamoja na Yanga dhidi ya JKT Tanzania ambapo Benard Morrison hakujiunga na timu licha ya kufanya mazoezi na timu pamoja na jina lake kujumuisha katika kikosi cha wachezaji watakao safiri na timu
Kupitia nakala iliyotolewa na klabu imesisitiza kuwa endapo kuna klabu yoyote inayomtaka mchezaji huyo benard MOrrison ifuate sheria na taratibu zote kwa maana Morrisn bado ni mchezaji halali wa Yanga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...