Na Said Mwishehe,Michuzi TV

WAENDESHA wa usafiri Bodaboda wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam wametakiwa kufuata sheria katika kutoa huduma hiyo ya kubeba na kusafirisha abiria kutoka eneo moja kwenda jingine.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Daniel Chongolo amesema hayo wakati akizungumza na Michuzi Blog, ambapo amefafanua kuwa kuna kila sababu ya kuhakikisha waendesha bodaboda wanazingatia sheria kwani wale ambao watabainika kukiuka watachukuliwa hatua.

Hata hivyo amesema kwa sasa hali ya usalama ni kubwa zaidi ndani ya Wilaya hiyo na hata matukio ya watu kuporwa bodaboda yamepungua."Hali ni nzuri sana kwasababu hata matukio makubwa yaliyokuwa yanatokea huko nyuma kwa saa hayapo tena".

Ametumia nafasi hiyo pia kuwaonya waendesha bodaboda ambao wanatumia usafiri huo kufanya matukio ya uhalifu na kuacha shughuli za kusafirisha abiria. "Waendesha bodaboda ambao nao wanakwapua waache kufanya hivyo mara moja.Tuwakamata na kuwachukulia hatua".

Wakati huo huo ametoa mwito kwa wananchi kuwa sehemu ya kufanikisha ulinzi katika maeneo yao , waache kupokea au kulinda watu ambao ni wahalifu kwenye maeneo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...