Na Zainab Nyamka
WAMEKAA!!! Mchezo wa Kirafiki kati ya Yanga na KMC imemalizika kwa Yanga kukubali kipigo cha goli 3-0.
Mchezo huo umechezwa leo katika Uwanja wa Uhuru ikiwa ni mchezo wao wa pili wa kirafiki baada ya kupata ushindi wa 3-1 dhidi ya Transit Camp.
Mpira ulianza kwa kasi KMC wakitawala mchezo kwa dakika za mwanzo kabla ya Yanga kubadilisha mchezo na kuonekana kuutawala.
Dakika ya 45 kabla ya mapumziko, KMC wanaandika goli pili kupitia kwa Ilanfya kwa pasi safi ya Emmanuel Mvuyekule.
Hadi mapumziko KMC wanatoka wakiwa mbele kwa goli 2-0 dhidi ya Yanga.
Hassan Kabunda anaiandikia KMC goli lingine akipiga faulo iliyomshinda mlinda mlango Metacha Mnata na kuiandikia KMC goli la tatu na la ushindi.
Hadi mpira unamalizika KMC walitoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 3-0.
Mchezo unaofuata wa Yanga utakuwa ni wa Ligi Kuu dhidi ya Mwadui ambapo ni mchezo wa Kiporo utakaochezwa katika dimba la Kambarage Mkoani Shinyanga.'
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...