Bilionea
mpya nchini Tanzania ambae ni Mchimbaji wa Madini Bw. Saniniu Laizer,
akisaini daftari la wageni wakati alipofika kutembelea banda la Wizara
ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake katika Maonesho ya 44 ya
Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Afisa
Tehama kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Maendaenda
akimuonesha Bw. Saniniu Lazier, mfumo wa kielektroniki unaoonesha
muenendo wa makusanyo ya Serikali kwa Taasisi zote za kwa kila siku
ikiwa ni njia ya kuongeza uwazi na kudhibiti makusanyo ya fedha za umma,
wakati alipotembelea banda la Wizara pamoja na Taasisi zake katika
Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Tehama kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Maendaenda
akimuonesha Bw. Saniniu Lazier, namna ya kufanya Malipo ya Huduma za
mbalimbali kwa kutumia (GEPG- App) ambayo inawawezesha watumiaji
kuhakiki namba ya malipo (Control Number), kutathmini na kulipa
malipo ya Serikali kupitia huduma ya simu za mkononi, wakati
alipotembelea banda la Wizara pamoja na Taasisi zake katika Maonesho ya
44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Afisa
Tehama kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Maendaenda
akimueleza Bw. Saniniu Laizer, namna Mfumo wa Kielektroniki wa Malipo ya
Huduma za Serikali ambavyo umeweza kupunguza gharama za ukusanyaji wa
mapato ya Serikali kwa kuondoa ada ya miamala kwa Taasisi za umma na
kuwezesha taarifa sahihi za mapato ya Serikali kupatikana kwa wakati,
wakati alipotembelea banda la wizara pamoja na taasisi zake katika
Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Mwandamizi Masoko na Uhusiano kwa Umma (PSPTB) Bi. Shamim Mdee,
akimueleza Bw Saniniu Laizer, kuhusu majukumu mbalimbali ya Bodi ya
PSPTB ikiwemo kusajili watoa huduma za ununuzi na ugavi, alipotembelea
banda la Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake katika maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Afisa
Habari kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Ramadhani Kissimba
(kushoto) akimuongoza Bw. Saniniu Laizer, kutembelea banda la Wizara
pamoja na Taasisi zake wakati alipotembelea banda hilo kujionea huduma
na elimu inayotolewa kwa umma wakati wa Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya
Biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha na Mipango).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...