Na Woinde Shizza , Michuzi Tv Arusha
Benki ya CRDB
imezindua rasmi mfumo mpya wa kidijitali "QR code"kwa kanda ya
kaskazini ambao unamuwezesha mteja wa benki hiyo kutoa maoni,
mapendekezo na mrejesho ambapo mteja atatumia simu janja kuweka maoni
kwenye sanduku la maoni tofauti na ilivyozoeleka.
Akizungumza
jijini Arusha mara baada ya kuzindua mfumo huo meneja wa bank hiyo
kanda ya kaskazini Chiku Issa amesema CRDB inakuwa ya kwanza kuzindua
mfumo huu ambao utawawezesha wateja kutoa maaoni ya huduma au malalamiko
moja kwa moja ambayo yatapokelewa na kujibiwa bila kusubiri.
Uzinduzi
huo ambao tayari umefanyika katika mikoa ya Dar es salaam na Mwanza kwa
mkoa wa Arusha umezinduliwa katika tawi la Arusha ambapo wateja wa
benki hiyo wamehudhuria na kushuhudia namna ambavyo mfumo huo
unavyofanya kazi kwa ufanisi.
“Hii
ni huduma ambayo itahakikisha wateja wetu wanakuwa karibu Zaidi na
benki na kupata huduma nyingi Zaidi na kutoa maoni yao yatakayoweza
kusaidia benki yetu iweze kuendelea vizuri”alisema Chiku.
Mkuu
wa kitengo cha huduma kwa wateja bank ya CRDB Yolanda Urio amesema
mfumo huo ni rahisi, salama na haraka kwa kuwa mteja hupata mrejesho
kwani mteja anachotakiwa kufanya ni kupakua application tu.
"Mfumo huu umeunganishwa na mifumo mingine na unampa fursa mteja wa CRDB kupata huduma mbalimbali " alisema Urio
Mmoja
wa wateja wa benki ya CRDB Charles Hotay amesema huduma hiyo ni
mkombozi kwao kwa sababu kuna nyakati mteja anahitaji utatuzi wa
changamoto fulani kwa haraka lakini walikuwa wanalazimika kwenda bank
kuuliza au kujaza fomu na kuweka kwenye kisanduku ambapo hatukujibiwi
kwa wakati.
Naye
Dina Patrick mteja aliyehudhuria kwenye uzinduzi huo amesema mbali na
kusaiidia wateja wa CRDB mfumo huu unamanufaa Zaidi kwa kuwa
utasaidia wanafunzi ambao mara nyingi hutumia mitandao kulipia huduma
mbalimbali na watakapo kwama ni rahisi kupata utatuzi.
Mkuu
wa kitengo cha huduma kwa wateja bank ya CRDB Yolanda Urio na viongozi
mbalimbali wa CRDB wakikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa mfumo mpya
wa QR CODE kwa kanda ya kaskaziniunaomuwezesha mteja kutoa maoni ya huduma au malalamiko moja kwa moja ambayo yatapokelewa na kujibiwa bila kusubiri
Meneja wa benki ya CRDB kanda ya kaskazini Chiku Issa akikata keki
katika uzinduzi wa mfumo mpya wa kidigital "QR CODE "katika hafla
iliyofanyika kwenye tawi la CRDB Arusha.(picha na Woinde Shizza).
Mkuu
wa kitengo cha huduma kwa wateja bank ya CRDB Yolanda Urio akimuelekeza
mteja wa benki hiyo Bw.Charles Hotay namna ya kutumia mfumo mpya wa
kutoa malalamiko kwa benk kwa haraka wa QR CODE(picha na Woinde Shizza )
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...