NA MWAMVUA MWINYI, BAGAMOYO
MKUU
wa wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani Zainab Kawawa, amemuweka ndani
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Makurunge ,Floliana Kaliamwe, kutokana na
matumizi mabaya ya fedha za Serikali.
Kawawa
alichukua hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na taarifa ya matumizi ya
shilingi milioni kumi za Halmashauri, zilizolenga kupauwa vyumba viwili
na ofisi shule ya awali Kitongoji cha Mkwajuni, huku Mbunge aliyemaliza
muda Dkt. Shukuru Kawambwa akitoa milioni moja ya kuweka kifusi.
Wananchi walilalamikia kukwama ujenzi huo tangu 2018, na kusema ujenzi huo asilimia kubwa umetumika kwa nguvu zao.
Alimhoji
Floliana ambaye alisema walipokea milioni 10 mwaka 2018 kwa ajili ya
upauaji huo, sanjali na milioni moja iliyotolewa na Dkt. Kawambwa kwa
ajili ya kifusi, ambapo Mkuu huyo hakuridhika na taarifa yake ndipo
akaamuru Polisi wamchukue.
"Sijaridhika
kabisa na taarifa ya matumizi ya fedha za serikali, ambazo ni kodi ya
wananchi, pia kigezo kipi kilichotumika kuletwa pesa hizo pasipokuwepo
kwa utaratibu wa matumizi ya fedha hizo?," alihoji Kawawa huku
akimuamuru Mkuu wa Polisi amchukue Mtendaji.
Aidha
Mkuu huyo amekerwa na Ofisa anayesimamia majengo katika Halmashauri kwa
kitendo chake cha kutofika eneo la miradi, hali inayoweza kuchangia
kutotekelezwa ipasavyo kazi zinazolenga kuondoa kero za wananchi kwa
ufasaha kulingana fedha zinazotolewa.
"Wataalamu
kipindi hiki sio cha kukaa maofisini, mnatakiwa kutembelea miradi
ambayo inapelekewa pesa za kodi zinazolipwa na wananchi, sipo tayari
kuona juhudi za rais wetu John Magufuli zikokwamishwa na watu wachache,"
alisema Kawawa mpaka kufikia kuto
Kawawa
alitoa onyo kali kwa watumishi wa Serikali wa ngazi mbalimbali
kutekeleza majukumu hao kwa weredi mkubwa, kwani hatokuwa tayari kuona
uzembe katika utekelezaji huo.
Mmoja
wa wasimamizi wa ujenzi huo alisema kuwa wao walitekeleza majumumu yao
ya kusimamia ujenzi huo, kwa kuanza kuweka mbao za kenchi kisha kupiga
bati katika vyumba hivyo vitatu vya shule hiyo, kwa lengo la kuwawezesha
watoto kuanza elimu ya awali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...