JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Dereva wa Basi la Kampuni ya Kyela Express DENIS LAMECK [48] aliyekuwa akiendesha Gari yenye namba za usajili T. 756 DEF Scania Basi baada ya kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha mtu mmoja aitwaye AIDA IPONJA [42] Mkazi wa Masukulu.
Ajali hiyo imetokea mnamo tarehe 16.07.2020 majira ya saa 22:20 Usiku huko Kijiji cha Kyimbila kilichopo Kata ya Mpuguso, Tarafa ya Pakati, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya katika barabara ya Tukuyu – Kyela ambapo Gari hilo Basi la Abiria Mali ya Kampuni ya Kyela Express lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Kyela iliacha njia na kupinduka na kusababisha kifo kwa abiria mmoja.
Aidha katika ajali hiyo abiria wanne walijeruhiwa ambao ni:-
  1. SALOME SHIMITA [43] Mkazi wa Kyela.
  2. SABINA JOSEPH [19] Mkazi wa Kyela.
  3. TALAMPE KANYENYE [41] Mkazi wa Kyela.
  4. PASCHAL MERIMERI [36] Mkazi wa Jijini Mbeya.
Majeruhi wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe Makandana. Chanzo cha ajali ni mwendo kasi katika eneo lenye mkungu na mvua. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitalini hapo. Upelelezi unaendelea.

KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO].
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia GWANTWA ELIAS [30] Mkazi wa Itunge Wilayani Kyela akiwa na pombe haramu ya moshi (gongo) ujazo wa lita 100.
Mtuhumiwa amekamatwa mnamo tarehe 16.07.2020 majira ya saa 09:30 Asubuhi huko Kijiji na Kata ya Itunge, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya. Mtuhumiwa ni muuzaji wa Pombe hiyo na atafikishwa mahakamani leo tarehe 17.07.2020.
                                                            Imetolewa na;
[ULRICH O. MATEI -SACP]

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...