MWANAHABARI Dotto Kahindi Mkenye maarufu kama 'Mandolin' leo 14 Julai, amechukua fomu ya kutia nia ya kugombea Ubunge Jimbo la Busanda kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM.

Dotto Kahindi Mkenye amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa CCM Wilaya ya Geita, Mwinyikheri Baraza.

Dotto Kahindi MKENYE ni Mwandishi wa Habari na Masimamizi wa Miradi mbalimbali ikiwemo ya Kilimobiashara, Ufugaji na Biashara.

Tasnia ya Habari amefanyakazi kama Mwandishi kwenye magazeti mbalimbali ikiwemo gazeti la Mwananchi la kampuni ya MCL, na amekuwa mtangazaji wa Radio pia. 

Mbali na Uwanahabari, amekuwa Meneja wa Programu kwenye Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania na sasa ni Meneja wa programu wa Taasisi ya Utamaduni na Maendeleo Africa Mashariki (CDEA).

Ni mwanzilishi wa shule ya Muziki ya Action Music Academy na ni mmiliki wa Promo Online Tv ambayo inatoa Habari za Kilimobiashara na Mazingira.

Dotto Kahindi MKENYE, leo amechukua fomu ya kutia nia ya kugombea Ubunge Jimbo la Busanda. Hapo akipokea fomu hiyo kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Geita, Mwinyikheri Baraza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...