Bi Hindu Lugome akikabidhiwa fomu za kuwania ubunge katika jimbo la Vunjo ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) akiwa miongoni mwa kundi la Wanawake 50 waliojitokeza kuwania ubunge kupitia majimbo ya mkoa wa Kilimanjaro.
Bi Hindu Lugome akikamilisha zoezi la ulipiaji wa ada kwa ajili ya fomu ya kuwania Ubunge ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Vunjo.
Bi Hindu akionesha fomu yake aliyochukua kwa ajili ya kuwania Ubunge katika jimbo la Vunjo ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Na Dixon Busagaga, Moshi
KUNDI la vijana ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka huu ni wazi limehasika baada ya kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu kwa lengo la kuwania nafasi ya kupewa ridhaa ndani ya chama hicho ya kupeperusha Bendera katika ngazi za majimbo.
Jina la Hindu Lugome si geni katika siasa za Jimbo la Vunjo ambapo katka uchaguzi wa mwaka 2015 ni miongoni mwa waliotia nia akiwa na umri mdogo wakati huo miaka 25 na sasa amerejea tena akiwa na umri wa miaka 30 akijaribu kutafuta nafasi hiyo kwa mara nyingine.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...