Mkuu wa Msafara uliowasindikiza Wakimbizi wanaorejea kwa hiari Burundi, ambaye ni Afisa Tawala wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Ngeze Ramadhani (Kulia). Akimkabidhi Mwakilishi wa Serikali ya Burundi Jules Bagayimpunzi (Kushoto), Nyaraka zinazowahusu Wakimbizi 176 waliorejea kwa hiari Nchini Burundi. Tukio hilo limefanyika leo katika Mpaka wa Tanzania na Burundi Manyovu Mkoani Kigoma na kuwashirikisha Serikali ya Tanzania, Burundi na Mashirika ya Kimataifa yanayohudumia Wakimbizi.  
 Mratibu wa Usalama wa UNHCR Mkoa wa Makamba Nchini Burundi, Cathie Monni (Kushoto), akibadilishana na Mwakilishi wa UNHCR Kigoma Nyaraka zinazohusu Wakimbizi wa Burundi 176 waliorejea Burundi leo kutoka Tanzania. Tukio hilo limefanyika leo katika Mpaka wa Tanzania na Burundi Manyovu Mkoani Kigoma na kuwashirikisha Serikali ya Tanzania, Burundi na Mashirika ya Kimataifa yanayohudumia Wakimbizi.  
 Baadhi ya wawakilishi wa Serikali ya Burundi na Watumishi wa Mashirika yanayohudumia Wakimbizi Nchini Tanzania, Wakiwatazama Wakimbizi waliomo ndani ya mabasi  manne waliyokuwa wakisafiria kutoka Nchini Tanzania kurejea kwa hiari Nchini kwao Burundi. Tukio hilo limefanyika leo katika Mpaka wa Tanzania na Burundi Manyovu, Mkoani Kigoma na kuwashirikisha Serikali ya Tanzania, Burundi na Mashirika ya Kimataifa yanayohudumia Wakimbizi.  
Baadhi ya wawakilishi wa Serikali ya Burundi na Watumishi wa Mashirika yanayohudumia Wakimbizi Nchini Burundi, wakiwa tayari kuwapokea  Wakimbizi 176 wa Burundi waliorejea kwa hiari nchini kwao leo. Tukio hilo limefanyika katika Mpaka wa Tanzania na Burundi Manyovu, Mkoani Kigoma na kuwashirikisha Serikali ya Tanzania, Burundi na Mashirika ya Kimataifa yanayohudumia Wakimbizi.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...