Na Said Mwishehe,Michuzi TV.

MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) katika Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam wamejitokeza kwa wingi kuanza kuchukua fomu za kuwania nafasi za ubunge ambapo jimbo la Temeke waliochukua fomu ni 38 wakati jimbo la Mbagala ni 41.

Akizungumza na Michuzi TV na Michuzi Blog leo Julai 14,2020, Katibu wa Siasa na Uenezi wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Ally Kamtande amesema kuwa katika Wilaya hiyo muamko wa wanaCCM kuchukua fomu za kuwania nafasi za udiwani, ubunge , pamoja na viti maalum kwa nafasi ya ubunge na udiwani imekuwa kubwa.

Amefafanua hadi jioni ya leo saa 10 jioni kwa nafasi ya ubunge ambao wamechukua fomu kwa Jimbo la Mbagala imefikia 41 na Temeke waliochukua fomu kuwania ubunge ni 38.

"Watia nia ambao wamechukua fomu za ubunge kwa Mbagala ni 41 na kati ya hao Temeke ni 38 na kati hao 38 wanawake ni wawili,"amesema Kamtande na kusisitiza kuwa baadhi ya watia nia waliochukua fomu wawili wamesharudisha fomu za kuwania ubunge ambapo mmoja anatoka Jimbo la Temeke na mwingine anatoka jimbo la Mbagala.

Hata hivyo ameendelea kusisitiza umuhimu wa watia nia waliochukua fomu na wale ambao watajitokeza kuhakikisha wanazingatia tararibu ambazo zimewekwa na Chama kwani kinyume na hapo watapoteza sifa.

"Tunawakumbusha watia nia wa nafasi zote wawe makini katika kufuata sheria, kanuni na taratibu ambazo zimewekwa.Huu sio wakati wa kampeni bali ni kipindi cha kuchukua na kurejesha fomu tu,"amesema Kamtande na kusisitiza hawatajii kusikia kauli zinazoashiria kuanza kampeni kabla ya wakati.

Kuhusu muamko watia nia kujitokeza kwa wingi Kamtande amesema kuna sababu nyingi lakini uwazi ambao umeoneshwa kwenye ngazi ya kitaifa ndani ya Chama hicho imekuwa chachu kubwa lakini pia utendaji kazi uliotukuka kwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa Dk.John Magufuli.

Hata hivyo watia nia kadhaa wamepata fursa ya kueleza sababu za kuchukua fomu za kuwania nafasi aidha kwenye udiwani au ubunge huku wakieleza kuwa kwa kuwa muda wa kampeni bado hujafika kwa sasa ni uchukuaji na urejeshaji fomu tu na baada ya hapo watakuwa na mengi ya kueleza kwa wananchi.
 Mtia nia wa nafasi ya udiwani wa Viti Maalum Kata ya Makangalawe Rebecca Eliazar akipata maelekezo ya jinsi ya kujaza fomu hiyo baada ya kuichukua leo Julai 14,2020 katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Temeke.
 Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Andrew Gwaje (kulia) akitoa maelekezo ya jinsi ya kujaza fomu ya kuwania ubunge kwa mtia nia ya ubunge Jimbo la Temeke Adil Mohamed jimbo
 Mtia nia wa jimbo la Temeke jijini Dar es Salaam Mwalim Kwame Kambulu(kushoto) akiwa amekabidhiwa fomu ya kuwania jimbo hilo la Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Andrew Gwaje(kulia).
 
Mtia nia wa nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Mbagala jijini Dar es Salaam Buluba Mabelele(kushoto) akikabidhiwa fomu ya kuwania jimbo hilo kutoka kwa Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Andrew Gwaje(kulia).
 Mtia nia wa nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Mbagala jijini Dar es Salaam Buluba Mabelele akijaza akiandika jina lake kabla ya kukabidhiwa fomu ya kuwania ubunge jimbo la Mbagala jijini Dar es Salaam baada ya kwenda kuchukua fomu hiyo katika ofisi za CCM wilaya ya Temeke.
 
Kada wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Nicholous Mpangala ambaye anawania jimbo la Temeke jijini Dar es Salaam akiipitia fomu hiyo ya kuwania nafasi hiyo baada ya kuichukua leo katika ofisi za Chama hicho wilayani Temeke.
 
Mtia nia wa nafasi ya Udiwani kata ya Kijichi Sabrina Rupia (kulia) akiwa ameshika fomu ya kuwania nafasi hiyo baada ya kwenda kuichukua leo katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Temeke.
 
Mtia nia katika jimbo la Temeke jijini Dar es Salaam Simon Ruago ambaye amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga akipata maelekezo kutoka kwa Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) Andrew Gwaje(kulia).
 
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga Simon Ruago akijaza moja ya nyaraka baada ya kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya ubunge jimbo la Temeke jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Siasa na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Ally Kamtande akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mchakato wa uchukuaji na urejeshaji fomu ambao umeanza leo ambapo ametumia nafasi hiyo kuwasisitiza watia nia wote kuzingatia sheria, kanuni na tararibu zilizowekwa na Chama hicho.
Katibu wa Siasa na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Ally Kamtande akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mchakato wa uchukuaji na urejeshaji fomu ambao umeanza leo ambapo ametumia nafasi hiyo kuwasisitiza watia nia wote kuzingatia sheria, kanuni na tararibu zilizowekwa na Chama hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...