Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
BAADA
ya kuacha chuo miaka 10 iliyopita Clayton Ward (30) amehitimu shahada
yake ya kwanza katika Chuo cha MassBay Community nchini Marekani huku
akitegemea kuwa mwalimu wa historia katika shule za Sekondari.
Clayton
ni dereva wa magari ya wanafunzi, ambaye familia yake wakiwemo wazazi
wake wamefanya kazi hiyo kisha na yeye akajikuta amekuwa dereva wa
wanafunzi ambao amekuwa akiwashirikisha namna anavyopenda somo la
historia kila alipokuwa akiwaendesha.
Kwa
mujibu wa Shirika la Utangazaji la CNN imeelezwa kuwa Clayton akiwa
anawaendesha wanafunzi katika mji wa Framingham, Massachusetts wengi wao
walikuwa wakimweleza waliyokuwa wakijifunza na alipokuwa na wanafunzi
wa sekondari waligundua kuwa Clayton ni mwanahistoria mzuri sana na
wakawa wanamuuliza maswali yahusuyo historia.
"Baadhi
ya watoto walitamani niwe Mwalimu wao na hiyo ni kutokana na mitazamo
tofauti na sauti tofauti na za walimu wao waliowazoea na maongezi yao
yanivuta na kunipa nguvu ya kurudi chuo na kutimiza ndoto yangu ya kuwa
mwalimu wa historia wa shule za Sekondari" Clayton Ameieleza CNN.
Clayton
alianza Chuo mwezi Mei 2019, akisoma masomo ya jioni na kwa njia ya
mtandao na hiyo ni baada ya kufanya shughuli yake ya udereva kwa nyakati
za mchana.
Ndani ya mwaka mmoja alimaliza masomo yake kwa ufaulu wa kiwango cha juu (GPA 4.0 kwa mujibu w Chuo.)
Clayton ameieleza CNN kuwa asingeweza kupata shahada hiyo bila ushawishi wa watoto hao.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...