DJ wa wasafi Rommy Jones a.k.a Rj the dj akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutambulisha Albamu ya 'CHANGES' hoteli ya Hyatt jijini Dar es Salaam leo.
Al-Hassan Muhidin, Michuzi Tv
DJ wa wasafi Rommy Jones a.k.a Rj the dj ametambulisha Album yake inayokwenda kwa jina la 'CHANGES'.
Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa albamu hiyo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam Rommy amesema katika albamu hiyo yeye hajaimba.
"Sijashiriki kwenye kuimba ila nimejaribu kukutanisha wasanii kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya Tanzania,"
Miongoni mwa walioshirikishwa kwenye albamu hiyo ni pamoja na Morgan heritage, Sho madjozi kutoka Afrika Kusini, Mbosso pamoja na mwanadada Zuchu kutoka kundi la Wasafi (WCB).
Aidha,Rommy amesema ndani ya Albamu hiyo kuna ladha tofauti tofauti za Muziki.
Hata hivyo ametangaza Agosti 16 itakua siku rasmi kuzinduzi albamu hiyo.
Pia amesema angependa kualika baadhi ya wasanii wa nje ila kutokana na janga la Covid 19 limesababisha kutokuepo kwao kutokana na nchi zao bado zipo kwenye Lockdown.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...