. Afisa Kilimo wa zao la mboga mboga kutoka Manispaa ya Kinondoni, Bwana. Emanuel Chacha akitoa maelezo ya Kilimo hicho kwa kutumia udongo kwa Wananchi waliofika katika Banda la Maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.
Mjasiriamali wa Samaki na Dagaa kutoka Manispaa ya Kinondoni, Bi. Mwajuma Mwinyimbe akitoa maelezo kwa Wananchi waliofika katika banda la Manispaa hiyo viwanja vya maonesho ya Wakulima Nanenane yanayoendelea Mkoani Morgoro.
Katibu
Tawala wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Bi. Mwanana Msumi, akipata
maelezo kutoka kwa Maafisa wa Kitengo cha Uchaguzi Manispaa ya Kinondoni
alipotembelea Banda hilo kwa lengo la kujionea maonesho hayo.
Mtaalamu wa kutengeneza mfumo wa kisasa wa ufugaji wa Samaki Bwana.
Jonas Ndau akitoa maelezo kwa Wananchi waliofika kuona mfumo huo
unavyofanya kazi.
Mtaalamu
wa ufugaji wa Samaki kwa kutumia njia ya Bwawa la maji kutoka Manispaa
ya Kinondoni, bwana Masumbuko Nzingula akitoa maelezo kwa Wananchi
waliofika katika Banda la Manispaa hiyo katika Viwanja vya Maonyesho ya
Nanenane mkoani Morogoro.
Muonekano wa zao la Nyanya lililolimwa kwa kutumia mfumo wa eneo la wazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...