Napenda kuungana na mamilioni ya Watanzania kumpongeza Dkt. John Pombe Magufuli kuchukua fomu ya kugombea urais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ninamtakia kila la heri airejeshe tayari kwa ushindi Octoba 28, 2020.

Nasema ushindi kwa maana kati ya wote tuliosikia wanagombea hakuna anayefikia hata robo ya uzalendo, uadilifu, uchapa kazi, ufuatiliaji na ucha Mungu alio nao Dkt. Magufuli ambao umetuvusha miaka mitano mpaka sasa tupo kwenye uchumi wa kati.

Dk. Magufuli ndio tumaini na tegemeo la pekee la Mtanzania mnyonge na maskini kwani amewawezesha kusoma bure shule ya Msingi hadi sekondari, amewajengea hospitali, vituo vya afya, Zahanati kila kona ya nchi na kuwaweka Madaktari, Madawa na vifaa tiba.

Ni Dkt. Magufuli huyu huyu ametupatia heshima Watanzania kwa kuhakikisha tunanunua ndege zetu wenyewe; tunajenga reli ya kisasa ya umeme ya SGR; tunajenga Bwawa kubwa la umeme utakaozalisha megawatts 2115; amejenga Miundombinu ya kisasa ya Madaraja, barabara, viwanja vya ndege na amehakikisha rasilimali zetu zinatunufaisha sisi Watanzania kuliko kipindi chochote kile.

Alipoona Wakulima wanaonewa aliingilia kati bei za mazao; Amehakikisha huduma kwenye ofisi za umma zinaimarika na leo hii hakuna tena matabaka wala uonevu wa Wenye nguvu kwa Wanyonge. Tumpate wapi tena kama Dk. Magufuli?

Tulianza na Mungu, tutamaliza na Mungu. Tumpe tena Rais Magufuli miaka mitano akakamilishe miradi ya ujenzi mIkubwa aliyoianza; Kama aliweza kutufikisha uchumi wa kati kwa muda wa miaka 5 tu, hadi 2025 nchi yetu ya Tanzania itakuwa kama Ulaya mpya. Itakuwa ni miaka 5 ya fursa, maendeleo, raha zaidi na utajiri kwani misingi imara na mizuri imeshawekwa.

- Emmanuel J. Shilatu
DO MIHAMBWE
0767488622
 
Mgombea wa Urais  Dkt. John Pombe Magufuli akionesha Ilani ya Uchaguzi wakati
akiongea na  wanachama wa CCM wa Dodoma baada ya kutoka kuchukua fomu
hizo za kugombea Urais kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi leo  jijini Dodoma
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...