Na Woinde Shizza, Michuzi Tv Arusha .
Kaimu Msajili wa bodi ya nyama Tanzania Imani
Sichalwe ameiomba serikali kununua ndege ya mizigo kwa ajili ya
kusafirisha nyama nje ya nchi kwani soko la nyama nje ni
kubwa sana
Sichalwe ameyasema hayo leo wakati
akizungumza na Waandishi wa habari ndani ya Banda lao lililopo katika maonesho ya
nane nane yanayofanyika katika viwanja vya Themi njiro jijini Arusha, Ambapo
alibainisha kuwa kuwepo kwa ndege ya mizigo kutasaidia kupunguza gharama ya
usafirishaji nje ya nchi
Alisema kuwa iwapo itakuwepo ndege ya Taifa kutakuwa na uhakika wa kago ya kusafirishia mizigo pia
itamsaidia kuimarisha biashara ya nyama nje ya nchi kwani mizigo ya nyama
itakuwa inafika katika nchi husika kwa wakati
Aidha pia alizitaka
Halmashauri zote hapa nchini kujenga viwanda pamoja na machinjio Bora ya nyama
ili nyama zinazopatikana hapo zisimamiwe vyema ziwe na ubora ambao unaweza
kuuzwa Ndani ya nchi nanje ya nchi .
“hapa nchini kwetu tuna
mifugo mingi sana ambayo tukiwa na viwanda vyetu pamoja na machinjio tukawa na
ndege yetu tukapeleka nje ya nchi tutapata
faida kubwa mno ambayo itasaidia kukuza pato la nchi yetu “alibainisha
Sichalwe
Aidha pia aliwataka
wananchi kujijengea tabia yakula nyama Mara kwa Mara kwani ulaji nyama kwa
wingi unasaidia mambo mengi ikiwemo kutengeneza akili ,unasaidia kutengeneza
vichocheo vingi vya mwili ,inakupa vitamini mbalimbali Kama vile zinki,ambapo
alibainisha kuwa binadamu waliubwa kula nyama Hivyo wanapaswa kula nyama ya
kutosha
Alifafanua kuwa kishe mtu
mmoja anatakiwa kula nyama kilo 50 kwa mwaka Ila hadi Sasa hapa nchini Tanzania
,mtu mmoja akila nyama nyingi kwa mwaka Ni kilo 15hivyo Ni vyema kila mtanzania
akajitaidi kula nyama nyingi kadri awezavyo ili afikie malengo
Alibainisha kuwa katika
kuelekea soko la kimataifa kila mfugaji
anatakiwa kufuga kisasa kwa kuacha kufuga mifugo mingi isiona tija badala yake
badala ya kufuga mifugo 2000 ambao akiwauza hapati faida ni boda mfugaji
akafuga mifugo kama 10 lakini ambayo ataweza kuihudumia vyema na akiipeleka
sokoni itampa faida kubwa zaidi
Wakati huo huo alitumia
muda huo kuwaonya wenye mabucha wote ambao bado wanatumia magogo kuuzia nyama
na kusema kuwa kwa sasa hivi kuna mashine maalumu ya kukatia nyama hivyo ni marufuku mwenye bucha yeyote kutumia
vigogo kukata nyama na iwapo atakutwa anatuia vigogo kufanya hivyo atalipishwa
faini ya shilingi laki moja au kuchukuliwa hatua zingine za kisheria.
Kaimu Msajili wa bodi ya nyama Tanzania Imani
Sichalwe akiongea na waandishi wa habari ndani ya banda lao la maonesho
lililopo katika viwanja vya Themi Njiro mkoani Arusha ,sehemu ambayo
maonesho ya 27 ya nane nane yanafanyika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...