NI wazi kuwa mapinduzi ya kidigitali yamekuwa na mabadiliko makubwa katika namna watu wanavyoishi kwenye miaka ya karibuni.

Kwa bahati nzuri, mabadiliko  haya yamekuja na fursa mbalimbali na pia yameipatia Tanzania nafasi ya kukuza uchumi wake Zaidi.

Katika ripoti yake ya hivi karibuni Benki ya Dunia iliainisha kuwa mapinduzi ya teknolojia ya kidigitali yataweza kupelekea mabadiliko zaidi juu ya namna watu wanavyofanya kazi duniani kote katika nyanja mbalimbali.

 Uchambuzi wao ulibainisha kuwa ufumbuzi wa kidigitali umesaidia kuchocheza ubunifu ikiwa ni pamoja na huduma za kifedha kwenye simu na ufanyaji biashara kidigitali.

Ifahamike kuwa kwa miaka kadhaa sasa, mapinduzi ya kidigitali yamekuwa jambo kubwa nchini Tanzania na katika miji kama Dar es Salaam imeona teknolojia ukikua zaidi na zaidi kila leo.

Ukuaji katika eneo hilo kwa  kiasi fulani kumechangiwa na jitihada zilizofanya na makampuni za mawasiliano nchini Tanzania kuwekeza katika sekta mbalimbali zinazokua.  Kwa ujumla, uwekezaji huu umekuwa na matokeo chanya  kwa wananchi, wafanyakazi na wafanyabiashara.

Kwa mfano, Huduma ya fedha kwenye simu ya Tigo Tanzania (Tigo Pesa) imezisaidia biashara kuwa na njia imara na ya haraka kuweka fedha, kutoa na kutuma fedha. Bila kuwa na ulazima wa kufika kwenye tawi la benki wafanyabiashara wanaweza kufuatilia miamala yao na kufanya malipo kwa wasambazaji bidhaa kwa urahisi zaidi.

Aidha, huduma ya Tigo Business ambayo ni maalum kwa ajili ya kuwasaidia wafanyabiashara wadogo na wa kati, imekuwa msaada mkubwa kwa biashara na wafanyakazi wake kufkia fursa za kibiashara. Kwa mfano, upatikanaji wa intaneti ya uhakika kwenye simu umekuwa na mchango mkubwa kusaidia biashara kutangaza biashara zao na huduma, pamoja na kuwasiliana na wateja wake. 

Licha ya faida hizo kufurahiwa na wateja wa Tigo kwa muda sasa, wengi wanaamini kuwa huduma hizo zitaanza kufurahiwa na wateja wa Zantel. Mwishoni mwa mwaka jana watoa huduma hao (Tigo na Zantel) walitangaza kusudio la kuungana. Mara muunganiko huo utakapokamilika wateja kutoka makampuni hayo wataweza kufurahia huduma zinazotolewa na kampuni zote mbili. 

Hii ina maana wateja wa Zantel  wataweza kutumia huduma kama Tigo Pesa na Tigo Business. Matarajio ya watumiaji wengi wa simu ni kuwa mchakato mzima wa kuungana kwa kampuni hizo utakamilika mapema ili wateja waweze kufurahia faida zake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...