Charles James, Michuzi TV.

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni na kwenye baadhi ya vyombo vya habari kwamba wapo wagombea wa nafasi za Ubunge na Udiwani waliopitishwa bila kupingwa.

NEC pia imesambaa hakuna pingamizi lolote lililotolewa kwa wagombea wa Urais wa vyama 15 ambavyo jana vilipitishwa na tume kugombea.

Akizungumza na wandishi wa habari katika Ofisi za Tume Njedengwa jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi, Dk Wilson Charles amesema tume bado haijatoa taarifa yoyote ya kutangaza mgombea wa mbunge au Udiwani ambaye amepitishwa bila kupingwa.

Dk Wilson amesema haiwezekani wawepo wagombea ambao wamepita bila kupingwa ilihali muda wa kuwekewa mapingamizi ambao kisheria ni kuanzia jana saa kumi jioni baada ya kupitishwa hadi leo saa kumi jioni.

" Kwa mujibu wa kifungu cha 40 (2) cha sheria ya Tume ya Uchaguzi sura ya 343 pingamizi linaweza kuwekwa kwa wagombea wa ubunge kama zuio kwa wagombea aliyeteuliwa kuanzia saa kumi jioni ya siku ya uteuzi hadi saa kumi jioni ya siku inayofuatia baada ya siku ya uteuzi.

Sasa ni jambo la kushangaza kuona vipo vyombo vya habari ambavyo vinatangaza uwepo wa wagombea waliopitishwa bila kupingwa kabla ya muda wa mapingamizi kuisha, tunawasihi sana ndugu zetu wanahabari kuepusha kutoa taarifa ambazo hazijathibitishwa na tume," Amesema Dk Wilson.
 Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Dk Wilson Charles Mahela akizungumza na wandishi wa habari leo jijini Dodoma

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...