Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
Wilaya ya Kinondoni Anna Luvanda, akizungumza na Kamati za ushindi za CCM Kata ya Makongo ka upande wa umoja huo, Dar es Salaam, leo. Kulia ni Katibu
wa UWT wa Wilaya hiyo Zahara Abdallah na kushoto ni Mwenyekiti wa UWT wa Kata ya Makongo Juu na Mgombea Udiuwani
Viti Maalumu, Janeth Mahawanga.
Mmoja na wanachana wa UWT Kata ya Makongo,
akichangia mada katika kikao hicho.
Wanachama wa UWT
wakicheza muziki baada ya kumaliza kikao hicho cha kimkakati.
Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV
UMOJA wa Wanawake Tanzania (UWT), wilayani
Kinondoni, jijini Dar es Salaam umeanza mikakati ya kuhakikisha Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kinapata ushindi mnono katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28 mwaka
huu .
Akizungumza katika mkutano wa ndani wa Kamati za ushindi za UWT , Kata ya Makongo Juu, wilayani humo, leo, Mwenyekiti wa jumuia hiyo wa Wilaya ya Kinondoni, Anna Luvanda, amesema wanawake ni jeshi kubwa linalotegemewa na Cha kupata ushindi, hivyo kuhimiza wanawake kujitokeza kwa wingi katika kupiga kura.
Ameongeza hakuna ubishi kuwa Mgombea Urais wa CCM Rais Dk. John Magufuli atashinda kwa kishindo ambapo pia nguvu kubwa ni kuona madiwani na nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kawe inarudi mikoni mwa CCM.
“Haiwezekani tukatawaliwa na Halima Mdee kwa miaka 15. Inatosha. Wanawake tusimame imara kuhakikisha mgombea wetu wa Ubunge, Askofu Josephat Gwajima inaibuka mshindi Kawe. Changamoto ni nyingi hapa, zinazotokana na usaliti uliofanywa na wenzetu mwaka 2015,”amesema Luvanda.
Amewataka wale wote ambao walitangaza nia na kura zao kuto kutosha, wasilete nongwa badala yake waungane kuunda timu za ushindi kwani CCM mbele mtu baadaye.
Kwa upande wake Katibu wa UWT wa Wilaya ya Kinondoni Zahara Abdallah, amesema muda wa kumng’oa Mdee jimbo la Kawe umefika na awamu hii ni lazima ang’oke kutokana na kushindwa kuwaletea maendeleo wananchi.
Wakati huo huo Mwenyekiti wa UWT wa Kata ya Makongo Juu ambaye pia ni mshindi wa nafasi ya Ubunge, Vitimaalumu, Janeth Mahawanga, amesema, Kata yake inakabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na kukosa mwakilishi na mtetezi wa wanawake, hivyo kuna kila sababu ya wanawake kuungana na kumng’oa Mdee ambaye ameshindwa kutetea wanawake.
Akizungumza katika mkutano wa ndani wa Kamati za ushindi za UWT , Kata ya Makongo Juu, wilayani humo, leo, Mwenyekiti wa jumuia hiyo wa Wilaya ya Kinondoni, Anna Luvanda, amesema wanawake ni jeshi kubwa linalotegemewa na Cha kupata ushindi, hivyo kuhimiza wanawake kujitokeza kwa wingi katika kupiga kura.
Ameongeza hakuna ubishi kuwa Mgombea Urais wa CCM Rais Dk. John Magufuli atashinda kwa kishindo ambapo pia nguvu kubwa ni kuona madiwani na nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kawe inarudi mikoni mwa CCM.
“Haiwezekani tukatawaliwa na Halima Mdee kwa miaka 15. Inatosha. Wanawake tusimame imara kuhakikisha mgombea wetu wa Ubunge, Askofu Josephat Gwajima inaibuka mshindi Kawe. Changamoto ni nyingi hapa, zinazotokana na usaliti uliofanywa na wenzetu mwaka 2015,”amesema Luvanda.
Amewataka wale wote ambao walitangaza nia na kura zao kuto kutosha, wasilete nongwa badala yake waungane kuunda timu za ushindi kwani CCM mbele mtu baadaye.
Kwa upande wake Katibu wa UWT wa Wilaya ya Kinondoni Zahara Abdallah, amesema muda wa kumng’oa Mdee jimbo la Kawe umefika na awamu hii ni lazima ang’oke kutokana na kushindwa kuwaletea maendeleo wananchi.
Wakati huo huo Mwenyekiti wa UWT wa Kata ya Makongo Juu ambaye pia ni mshindi wa nafasi ya Ubunge, Vitimaalumu, Janeth Mahawanga, amesema, Kata yake inakabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na kukosa mwakilishi na mtetezi wa wanawake, hivyo kuna kila sababu ya wanawake kuungana na kumng’oa Mdee ambaye ameshindwa kutetea wanawake.
Mwisho..
CAPTION
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...