Mapema leo Kamishna wa Operesheni
na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini,CP Liberatus Sabas(kushoto)
amewasili mkoani Morogoro kwaajili ya ukaguzi wa utayari kwa Askari
mkoani humo katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa Rais,
Wabunge na Madiwani,(kulia) Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Wilbroad
Mutafugwa (PICHA NA JESHI LA POLISI)
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini, CP
Liberatus Sabas akikagua Paredi la kutuliza ghasia (riot drill )paredi
hilo limeundwa na askari Polisi kutoka Mkoa wa Morogoro wakati wa
mazoezi ya utayari kwaajili ya kukabiliana na uhalifu. (PICHA NA JESHI
LA POLISI)
Kamishna
wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini, CP Liberatus Sabas
akizungumza na Maofisa na Askari Polisi wa vyeo mbalimbali mkoani
Morogoro baada ya kukakugua mazoezi ya utayari yaliyofanywa na askari wa
mkoani humo.CP Sabas amewataka Maofisa na askari hao kufanya kazi kwa
bidii na kwa weredi kwa lengo la kuhakikisha nchi inaendelea kuwa kisiwa
cha amani. (PICHA NA JESHI LA POLISI)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...