Mgombea wa Urais ,Yeremia Kulwa
Maganja akikabidhiwa Begi lenye Fomu ya Kugombea nafasi ya Urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha NCCR MAGEUZI katika
Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28 Oktoba, 2020 na Mwenyekiti wa Tume
ya Taifa ya Uchaguzi NEC Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage katika Ofisi
za Makao Makuu ya NEC Njedengwa jijini Dodoma.
Mgombea wa Urais ,Yeremia Kulwa
Maganja wakionyesha Mikono juu wakiwa na Begi lenye Fomu ya Kugombea
nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha
NCCR MAGEUZI katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28 Oktoba, 2020
pamoja na Mgombea Mwenza Haji Ambar Khamis mara baada ya kuchukua Fomu
hizo katika Ofisi za Makao Makuu ya NEC Njedengwa leo jijini Dodoma.
Mgombea wa Urais ,Yeremia Kulwa
Maganja kupitia Chama cha NCCR MAGEUZI katika Uchaguzi Mkuu
utakaofanyika tarehe 28 Oktoba, 2020 akisaini Kitabu mara baada ya
kuchukua Fomu hizo za Kugombea Urais katika Ofisi za Makao Makuu ya NEC
Njedengwa leo jijini Dodoma kulia ni Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) Dk. Wilson Mahera Charles.
Mgombea Mwenza kupitia Chama cha
NCCR MAGEUZI Haji Ambar Khamis akisaini kitabu katika Ofisi za Makao
Makuu ya NEC Njedengwa leo jijini Dodoma.
Sehemu ya wafuasi wa chama cha
NCCR MAGEUZI walipomsindikiza Mgombea wa Urais ,Yeremia Kulwa Maganja
kupitia Chama cha NCCR MAGEUZI katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe
28 Oktoba, 2020 katika Ofisi za Makao Makuu ya NEC Njedengwa jijini
Dodoma
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...