Taarifa zinasema kwamba mwanamke huyo aliuwawa na wanaume waliokuwa wamevalia sare za kijeshi kaskazini mwa nchi hiyo eneo lililokuwa na machafuko.
Haya yanajiri wakati ambapo serikali ya Msumbiji inajaribu kujiondolea lawama kwa kuwanyoshea kidole cha lawama magaidi ambao wamekuwa wakifanya mashambulizi katika mkoa wa Cabo Delgado.
Kuliibuka mkanda wa video wiki hii uliowaonyesha wanaume waliovaa sare za kijeshi wakimpiga mwanamke waliyemtuhumu kwa kuwa mwanamgambo na kisha baadae kummiminia risasi. Serikali imesema itauchunguza mkanda huo wa video.
"Wanajeshi wanne tofauti walimpiga risasi jumla ya mara 36 na aina ya bunduki za Kalashnikov na bunduki aina ya PKM," Amnesty ilisema, ikitaka "uchunguzi huru ufanyike".
"Video hii ya kutisha bado ni mfano mwingine mbaya wa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu na mauaji yasiyo na huruma yanayofanyika Cabo Delgado na vikosi vya usalama vya Msumbiji," alisema Deprose Muchena, Mkurugenzi wa Amnesty International kwa Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...