AZAM FC  KUMENYENA NA COASTAL UNION CHAMAZI KESHO.


Na Agness Francis,Michuzi Tv.



Kikosi cha Azam FC

Na Agness Francis, Michuzi Tv.

KIKOSI  cha Azam  fc kesho kinashuka dimbani  kuumana na wagosi wa kaya Coastal Union kutoka Jijini Tanga  katika muendelezo wa kinyanganyiro cha kombe la ligi kuu Vodacom Tanzania bara.

Mtanange huo wa aina yake wanalamba lamba Azam FC  watawakaribisha vijana kutoka Tanga coastal union katika uwanja wa Azam complex  Chamazi, majira ya saa moja jioni kwa kiingilio cha  shilingi 3000  kwa majukwaa ya mzunguko na 10000 kwa VIP.

Msimu huu michezo ya raundi ya kwanza  Azam fc ametoka kifua mbele  wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani ambapo mchezaji  Obrey Chirwa aliifungia timu yake bao 1-0 dhidi ya Polisi Tanzania,

Nao  wagosi wa kaya Coastal Union hali ilikuwa mbaya kwa upande wao,ambapo  walipoteza mchezo wake wa kwanza kwa matokeo ya 0-1 dhidi ya Namungofc katika uwanja wa Majaliwa  Lindi.

Tujikumbushe katika michezo  ya ligi kuu  iliyoisha msimu 2019-20 Azam alionekana kuwa kibonde wa  Coastal Union kwa kushindwa kufurukuta kupata alama 6 si nyumbani wala ugenini.

Mchezo wa raundi ya kwanza Azam akiwa ugenini katika dimba la uwanja wa Mkwakwani Mkoani Tanga iliruhusu nyavu zake kutikiswa na Coastal Union kwa  kufungwa bao 1-0 na kuondoka  wakiwa hawajaambulia kitu.

Huku mchezo  wa raundi pili pia Azam alipoteza tena  alama 3 muhimu wakiwa katika uwanja wa nyumbani Azam complex kwa kutundikwa mabao 2 -1 na wagosi wa kaya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...