Na Lusajo Frank, Dsj

MSHAMBULIAJI Nyota wa timu ya taifa ya Ureno, Cristian Ronaldo Dos Santos Aveiro {Cr 7} amefanikiwa kufikisha magoli 101 katika timu ya taifa.

Cristian Ronaldo aliweka kambani magoli mawili katika mchezo dhidi ya Sweden uliopigwa katika dimba la Friends Arena mjini Solna Sweden.

Ureno iliibuka na ushindi wa magoli wa mawili kwa sifuri dhidi ya Sweden, katika michuano ya ligi ya timu za taifa  (UEFA national league).

Ronaldo anakuwa mchezaji wa pili kufunga zaidi ya mabao 101 katika michezo 165 ya timu taifa na mchezaji namba moja ulaya, huku rekodi hiyo ikiwa bado inashikiliwa na Ali Daei, raia wa Iran akiwa na magoli 109.

Cristian Ronaldo anahitaji magoli 8 kuvunja rekodi ya mfungaji bora wa muda wote kwenye mechi za kimataifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...