Pichani ni walengwa kijiji cha Badugu wakipewa maelekezo na uongozi wa serikali ya kijiji kuhusu utaratibu wa malipo ya awamu ya kwanza TASAF III Kipindi cha pili. 

………………………………………………………………………………… 

Jumla ya kaya 3,065 Wilayani Busega zimefaidika na mpango wa kunususru kaya masikini TASAF III kipindi cha pili, huku jumla ya shilingi milioni 219,808,000 zikitolewa na serikali kwaajili ya malipo ya kwanza ya awamu ya tatu kipindi cha pili, hayo yamebainishwa na mratibu wa TASAF Wilaya ya Busega, Bi. Wema Mmari. 

Mpango wa TASAF awamu ya tatu kipindi cha pili, umetekeleza malipo ya kwanza Wilayani Busega kwa walengwa kulipwa fedha ambapo malipo yamefanyika kuanzia tarehe 23 hadi 25 Septemba, 2020. Malipo hayo yamefanyika huku walengwa wakitoa ushuhuda na kuishukuru serikali kwa utekelezaji wa kipindi cha pili wa TASAF III. 

Awali mratibu wa TASAF Wilaya ya Busega Bi. Wema Mmari alisema malipo hayo yamefanyika kwa kaya lengwa zote ambazo zilifanyiwa uhakiki katika zoezi lililofanyika mapema mwezi Julai mwaka huu. Malipo ya kwanza ya TASAF III kipindi cha pili yamejumuisha malipo ya mwezi Julai hadi Oktoba mwaka 2020. 

Jumla vijiji 41 kati ya 59 vilivyopo kwenye mpango wa TASAF Wilayani Busega vimefaidika na mradi wa TASAF III kipindi cha pili, huku walengwa wakiaswa kutumia fedha hizo kwaajili ya shughuli za maendeleo ili kuondokana na umasikini. 

Sehemu ya walengwa wameishukuru na kuipongeza serikali kwa kuendelea kujali kaya masikini kwani kwa kupitia TASAF kaya nyingi zimepiga hatua kiuchumi. Baadhi yao wamejikita katika shughuli za ufugaji, kilimo, na kununua mahitaji ya vifaa vya shule kwa watoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...