Na Mwandishi wetu, Babati 

MTUMISHI wa Baraza la ardhi na nyumba Wilaya ya Babati Mkoani Manyara, Ruth Semkuyu amefikishwa kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya hiyo kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa ya shilingi 100,000 kwa ajili ya kukazia hukumu. 

Semkuyu alifikishwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kwenye mahakama hiyo jana mjini Babati mbele ya hakimu Simon Kobelo. 

Mwendesha mashtaka wa TAKUKURU Evelyine Onditi akisoma hati ya mashtaka ya kesi hiyo ya jinai namba 155/2020 amesema Semkuyu ametenda kosa hilo akiwa ofisini kwake mjini Babati. 

Onditi amesema Semkuyu akiwa kwenye ofisi ya baraza la ardhi na nyumba Wilaya ya Babati aliomba rushwa kwa mkazi wa eneo hilo ili kukaza hukumu baada ya kushinda kesi yake kwenye baraza la kata. 
 
Amesema Semkuyu alitenda kosa hilo kinyume cha kifungu cha 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

Hata hivyo, Semkuyu alikana shtaka hilo mahakamani hapo alipoulizwa na Hakimu Kobelo kama ni kweli ametenda kosa hilo la kuomba na kupokea rushwa ya shilingi laki moja. 

Mshtakiwa huyo amepelekwa rumande kwenye gereza la mkoa huo la Mrara, mara baada ya kushindwa kutimiza masharti ya kupata dhamana. 

Hakimu Kobelo anayeshikilia kesi hiyo ameahirisha hadi Septemba 23 mwaka huu itakapotajwa tena mahakamani hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...