Tarehe 27 Septemba, 2020 Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya ametembelea mabanda ya Wizara ya Madini kwenye Maonesho ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayoendelea katika Uwanja wa Kituo cha Uwekezaji Bombambili Geita Majini .
Mara baada ya kutembelea Banda la Tume ya Madini kwenye maonesho hayo amepongeza kazi nzuri iliyofanywa na wataalam wa Tume na kuwataka kuendelea kuelimisha umma  hasa wachimbaji wadogo kuhusu Sheria ya Madini na kanuni zake, usalama wa afya na mazingira wanapoendesha shughuli za uchimbaji wa madini na biashara ya madini.

Aidha ameelekeza elimu kuhusu ushirikishwaji wa watanzania kwenye Sekta ya Madini kuendelea kutolewa ili kutoa fursa kwa wananchi wengi kushiriki kwenye sekta ya Madini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...