Sehemu ya Matofali yaliotolewa na Tretem Network of School 

Ujenzi wa moja ya Darasa ukiendelea
……………………………………………………………………….
NA FARIDA SAIDI,MOROGORO. 

Katika kuunga mkono juhudi zinzofanywa na serikali,Jamii imetakiwa kuchangia miradi ya maendeleo inayofanywa katika maeneo hususani miradi ya elimu ili kuwapa fursa watoto kusoma katika mazingira mazuri na salama yatakayochochea ufauru. 

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaaji wa Tretem Network Of School Geofrey Chami wakati anakabidhi matofali miatano(500) kwa Mkuu wa shule ya msingi shikizi ya Tungi iliopo kata ya Tungi Manispaa ya Morogoro,ambapo tofali hizo zitasaidia kumaliza kujenzi wa dalasa moja ambalo lipo katika kahatua ya awali. 

Aidha amewataka wadau wengeni kujitokeza katika kusaidia ujenzi wa madarasa yaliobaki pamoja na mahitaji mengine yanayohitajika katika shule hiyo ikiwemo madawati,huku akisema jukumu la kuhakikisha watoto wanasoma katika mazingira salama ni wote nasio serikali pekee. 

Kwa upande wao Mkuu wa shule hiyo na Mwenyekiti wa mtaa wameishuru Taasisis ya Tretem Network Of School kwa kutoa matofali hayo ambayo wanaamini yatakuwa chachu ya kuwasukuma wadau wengine kusaidia shule hiyo shikizi.

Hata hivyo shule hiyo ni shikizi kutoka shule ya msingi tungi ambayo ndio shule mama na imeanzishwa hivi karibuni kwa lengo la kuwasidia watoto wanasoma umbali mrefu katika kata hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...