Mwakilishi wa Vodacom Tanzania
PLC, Rehema Kipanga (katikati) akimkabidhi medali ya ushindi wa pili
mchezaji wa Namungo, Jamali Issa Dullazi mara baada ya mchezo wa Ngao ya
jamii uliofanyika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha jana ambapo
mshindi alikuwa timu ya Simba, mchezo huo ulitumika pia kuzindua msimu
mpya wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania. Kulia ni mkuu wa mkoa wa Arusha
Idd Hassan Kimanta.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni
na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akikabidhi Ngao ya
jamii kwa Nahodha wa Simba Sc, John Bocco mara baada ya kutwaa Ngao hiyo
ya kuashiria uzinduzi rasmi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
2020/21. Kushoto ni mkuu wa mkoa wa Arusha Idd Hassan Kimanta.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...