Na Mwandishi wetu, Mirerani
WATANZANIA
wametakiwa kusamehe ili waweze kupata amani mioyoni mwao kwa kujiepusha
na magonjwa na kuwa karibu na Mungu katika maisha yao ya kila siku.
Wito
huo umetolewa leo Septemba 13 Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro
Mkoani Manyara na Padri Elias Kimaro wa Kanisa Katoliki Parokia ya
Bikira Maria Mama wa Rozali Takatifu kwenye Dominika ya 24 ya mwaka A wa
Kanisa.
Padri Kimaro
amesema msamaha ni tiba ya moyo hivyo watanzania wanapaswa kutoa msamaha
kwa wote waliowakosea ili waanze ukurasa mpya wa maisha mioyoni mwao.
Amesema
msamaha huleta amani, umoja na utulivu kwani vita na vurugu hutokea kwa
sababu ya jambo dogo kushindwa kusameheana na kuanza maisha upya.
Amesema
wanapaswa kujifunza kusamehe kwani msamaha ni tiba ya moyo kuliko
kubeba mizigo ya kukumbuka makosa ya zamani ambayo huwezi kuyarekebisha
zaidi ya kusamehe.
"Unakuta
mtu amekukosea anaishi kwa furaha, lakini wewe badala ya kusamehe
unabeba moyoni na kupata ugonjwa wa moyo, kisukari kisha unakufa kwa
kuweka vitu kifuani," amesema Padri Kimaro.
Amesema
Mungu ni mwema anawasamehe binadamu pindi wanapokosea hivyo binadamu
nao wanapaswa kusamehe bila kuhesabu ni mara ngapi amefanya msamaha.
"Neno
la Injili ya leo kwenye kitabu cha Mathayo 18:21 linatufundisha namna
Yesu alivyotufundisha kusamehe saba mara sabini nasi tusamehe wakosaji
wetu kama Mungu anavyo tusamehe," amesema Padri Kimaro.
Amesema
tangu mtu azaliwe, awe kijana hadi kuwa mzee amefanya dhambi nyingi
lakini Mungu amesamehe kwani nini binadamu asimsamehe mwenzake.
"Msamaha
una hatua nyingi ikiwemo ya kwanza, ya pili na kuendelea hivyo kwa
kuanzia anza kujisamehe wewe mwenyewe kwa makosa uliyoyafanya kipindi
kilichopita na kuanza upya," amesema Padri Kimaro.
Padri Elias Kimaro wa Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira
Maria Mama wa Rozali Takatifu ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani
Simanjiro Mkoani Manyara, akiongoza sala ndani ya ukuta unaozunguka
migodi ya madini ya Tanzanite hivi karibuni.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...