Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

Hii sasa sifa!!! Kutokea Mikocheni hadi Kimbiji, kikosi cha timu ya Yanga kwa sasa wanatarajiwa kuhamia Kimbiji katika kambi mpya wakitokea Mikocheni.

Hatua hiyo inakuja baada ya mdhamini wao GSM kuamua kuwabadilishia kambi na kuwapeleka nje ya mji ili kupata muda zaidi wa kujifua na Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kambi hiyo mpya ya Yanga ina mahitaji yote ikiwemo Uwanja wa mazoezi wa mpira wa miguu, Kikapu na michezo mingine.

Mabadiliko hayo yanafanyika muda mfupi kabla ya kuanza kwa Ligi msimu 2020/21 siku ya Jumapili wakitokea katika kilele cha siku ya Mwananchi.

Yanga ilifanya kilele cha siku ya Mwananchi siku ya Jumapili Agosti 30, na kuweka historia ya kujaza uwanja pamoja na kuwa tamasha lililovutia na kufana likonogeshwa na Msanii Harmonize huku wakicheza Mchezo wa Kirafiki dhidhi Agle Noir.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...