Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Victor Ayo (katikati) akikata utepe kuashirikia uzinduzi wa Kivuko cha Barabara kwa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Victor Ayo (Aliyevaa Sare za Kaki) akivuka katika Kivuko hicho cha Barabara baada ya uzinduzi, Shule ya Msingi Wailes iliyopo Temeke jijini Dar.
Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes waliohudhuria uzinduzi wa Kivuko hicho
Baadhi ya Walimu wa Shule ya Msingi Wailes wakiwa katika uzinduzi wa Kivuko hicho cha Barabara

 Meneja Miradi kutoka AMEND, Simon Kalolo akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya uzinduzi wa Kivuko hicho Shule ya Msingi Wailes na jitihada za Shirika hilo katika uboreshaji wa Miundombinu ya Barabara.


Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

SHIRIKA linalojishughulisha na kuzuia ajali Barabarani  nchini (AMEND) limeendelea na jitihada zake za uboreshaji wa Miundombinu ya Barabara kwa kuboresha kivuko kwa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Wailes iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika uzinduzi wa Kivuko hicho, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Mrakibu Msaidizi wa Polisi, Victor Ayo amewapongeza AMEND kwa jitihada hizo za uboreshaji wa Miundombinu hiyo hususan kwa Shule za Msingi kwa Watoto wenye Mahitaji maalum.

Kamanda Ayo amesema ubunifu huo ni mkubwa baada ya kuona kivuko cha awali hakijakidhi vigezo, amesema Jeshi la Polisi litaendelea kuunga mkono jitihada za AMEND kuhakikisha Wanafunzi na Watu wenye mahitaji maalum kuwa na amani wanapovuka barabara.

Ametoa wito kwa madereva kutii sheria wanapofika katika Vivuko hivyo (Zebra Crossing) ili kuwapa nafasi Wanafunzi na Watu wenye mahitaji maalum kuvuka kwa amani pale wanapohitaji kuvuka katika maeneo hayo ya vivuko.

Pia Meneja Miradi kutoka AMEND, Simon Kalolo amesema wameshirikiana na Serikali upande wa TARURA, Ofisi ya Mkurugenzi na Jeshi la Polisi kuhakikisha Wanafunzi hao wa Wailes na Watu wenye mahitaji maalum  wanapata kivuko hicho sambamba na kutoa elimu kwa Madereva kuwajibika ipasavyo kufuata sheria wanapofika katika vivuko husika. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Usalama Barabarani Taifa, Kwa watu wenye Ulemavu, Ditram Kabatele amewapongeza AMEND kwa juhudi zao na kuwataka zoezi hilo kufanyika nchi nzima, amesema watawapa ushirikiano popote pale watakapohitaji. Amesema Vivuko hivyo vimepunguza idadi ya ajali kwa Wanafunzi na Watu wenye mahitaji maalum.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Wailes, Mwl. Jaribu Bakari amesema ujenzi wa Kivuko hicho utasaidia kwa kiasi kikubwa kwa Wanafunzi wa Shule hiyo kwa kuondoa adha ya kuvuka pale wanapoingia au kutoka maeneo ya Shule.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...