Na Said Mwishehe,Michuzi TV
CHAMA
Cha Mapinduzi( CCM) kimesema kwamba leo Oktoba 14 mwaka huu wanamliza
awamu ya tano ya kampeni zao na kuzindua rasmi awamu ya sita ya kampeni
zao ambazo ndio za salama huku kikitumia nafasi hiyo kuwaomba wakazi wa
Dar es Salaam kuhakikisha Oktoba 28 mwaka huu wanamchagua mgombea urais
wa Chama hicho Dk.John Magufuli.
Akizungumza
leo Oktoba 28,2020 mbele ya maelfu ya wananchi wa Majimbo ya Kawe na
Kinondoni jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)
Dk.Bashiru Ally amesema ratiba yao imepangwa kimkakati.
Dk.Bashiru
amesema awamu ya sita ambayo wanaizundua leo kwa Mgombea wao kufunga
kampeni zake jijini Dar es Salaam na kuelekea mikoa mingine ,ndio awamu
ya lala salama ambayo wana CCM wanajipanga zaidi kuelekea Oktoba 28
ambayo ni siku ya uchaguzi mkuu.
"Leo
tunamaliza awamu ya tano na kungia awamu ya sita ya kampeni zetu, bdii
awamu ya kupanga mawakala katika vituo vya uchaguzi, ndio awamu ya
kutafuta wapiga kura, ndio awamu kuelekeza wapiga kura jinsi ya kupiga
kura, awamu ya mabalozi wetu kutafuta kura na ndio wakati wa kuchukua
silaha zetu zote. Ndio awamu ya lala salama,"amesema Dk.Bashiru.
Hata
hivyo amesema wakati wakiendelea na kampeni zao,kuna mgombea urais wa
upinzani amekuwa akijifanya anaijua vizuri ratiba ya mgombea urais wa
CCM, hivyo wamemtaka mgombea huyo aache kugusa mitambo ya ushindi wa
Chama hicho
"Mgombea hu
yo anajifanya anapanga ratiba ya mikutabo ya mgombea urais wa CCM,n kwa
jinsi anavyoijua ratiba yetu tunadhani anakaibia kuja CCM,
tunamkaribisha.Tunachotaka kusema mwaka huu wapinzani watachapwa sana,
CCM na mgombea wetu wa urais tunakwenda kushinda kwa kura nyinyi Oktoba
28 mwaka huu,"amesema Dk.Magufuli.
Ametumia
nafasi hiyo kufafanua Dk.Magufuli katika uchaguzi mkuu mwaka huu ndio
mgombea mwenye kazi ngumu kwani anafanya kazi zaidi ya moja ba zote
amezifanya vizuri.
Pamoja
na hayo amesema kuwa Jiji la Dar es Salaam ndilo kitovu cha ukombozi
kwa nchi za barani Afrika, Dar es Salaam ndio wakombozi wa Taifa la
Tanzania kiuchumi kwani hata mapato mengi yatokanayo na kodi jiji hilo
linaongoza.Pia hata katika idadi ya wapiga kura Dar es Salaam ndio
inaongoza kuwa na wapiga kur wengi kulko sehemu nyingine yoyote nchini.
"Tuhakikishe
katika Oktoba 28 mwaka huu thugs Dk.Magufuli ashinde kwa kishindo,
Tuchague wagombea ubunge na madiwani wa CCM,"amesema Dk.Bashiru na
kuongeza Dk.Magufuli amesimama imara kuleta maendeleo ya nchi yetu hana
wa kushindana naye na wala hakuna anayemfikia kwa sifa alizonazo kwa
nafasi ya urais.
Kuhusu
kumbukizi ya Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye
aliyefariki dunia Oktoba 14,mwaka 1999 na kwamba ikifika mwaka 2022
Mwalimu Nyerere atakuwa anafikisha miaka 100 tangu atoke kwenye tumbo la
mama yake.
"Mwalimu
Nyerere anatimiza miaka 21 ya kifo chake, na itakapofika mwaka 2022
atakuwa anafikisha miaka 100 tangu azaliwe.Mwalimu Nyerere alisema bila
CCM imara nchi itayumba na chini ya Dk.Magufuli CCM iko imara sana na
anaishi katika maono ya Mwalimu Nyerere,"amesema Dk.Bashiru.
Amesema
kwa Dk.Magufuli amekuwa akiishi katika maono ya Mwalimu Nyerere na
amekuwa na sifa lukuki na miongoni kwa sifa hizo ni namna ambavyo
amekuwa akisimamia rasilimali za nchi na tukio la jana la kupokea gawio
la Sh.bilioni 100 kutoka sekta ya madini imethibitisha kwa vitendo Rais
Magufuli anavyosimamia vema rasilimali zq nchi.
"
Dk.Magufuli ana sifa ya kufanya kazi na maendeleo na hata katika
mahusiano ya watu ni.makubwa chini ya uongozi wako, umekuwa ukisema
maendeleo hayana Chama bali ni ya watu,"amesema.
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John
Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Jimbo la Kawe katika mkutano
wa Kampeni za CCM zilizofanyika katika uwanja wa Tanganyika Packers
uliopo Kawe, Kinondoni mkoani Dar es Salaam leo tarehe 14 Oktoba 2020.


Wananchi wa Jimbo la Kawe wakiwa
wamefurika katika Uwanja wa mkutano wa Tanganyika Packers kumsikiliza
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John
Pombe Magufuli leo tarehe 14 Oktoba 2020.
Mgombea
Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli akiwasili katika uwanja wa Tanganyika Packers kwa ajili ya
kuwahutubia wananchi wa Jimbo la Kawe leo tarehe 14 Oktoba 2020.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...