Muonekano wa sehemu ya chini ya meli ya MV Mwanza inayojengwa  jijini Mwanza na Mkandarasi GAS Entec kutoka Korea ya Kusini meli hiyo inayotarajiwa kukamilika mwakani  itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1200, tani 400 za mizigo na magari zaidi ya 20 itakapokamilika

Muonekano wa bodi la meli ya MV Mwanza inayojengwa jijini Mwanza na Mkandarasi GAS Entec kutoka Korea ya Kusini meli hiyo inayotarajiwa kukamilika mwakani  itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1200, tani 400 za mizigo na magari zaidi ya 20 itakapokamilika.

Mtaalam wa masuala ya ujenzi wa meli Mhandisi. Beda Patrick akifafanua jambo kwa  timu ya wahandisi toka Bodi ya usajili wa wahandisi nchini (ERB), walipokagua ujenzi wa meli hiyo jijini Mwanza.

Msajili wa wahandisi nchini Mhandisi. Patrick Barozi (mwenye fulana nyekundu), akisisitiza jambo kwa wahandisi waliopata fursa katika mradi wa ujenzi wa meli ya MV Mwanza kujifunza kikamilifu ili kupata ujuzi wa kutosha katika ujenzi huo (wa kwanza kushoto kwake), ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt.  Phillis Nyimbi akifuatilia kwa makini.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Meli nchini (MSL,) Bw. Erick Hamis akifafanua jambo kwa timu ya wahandisi toka Bodi ya usajili wa wahandisi nchini (ERB,) walipokagua maendeleo ya ujenzi wa meli ya MV Mwanza inayotarajiwa kukamilika mwakani na kutoa huduma katika ziwa Victoria.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...