MUSOMA, MARA
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewaonya baadhi ya wanasiasa nchini kuacha kuwatumia vibaya wananchi hususan vijana hasa katika kipindi hiki cha kampeni za kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 2020 na kuwaingiza kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani.
IGP Sirro amesema hayo akiwa Musoma mkoani Mara kwenye kikao kilichowahusisha viongozi wa kisiasa wakiwemo wagombea wa nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu waliopo mkoani humo ambapo aliwataka wagombea hao kutumia majukwaa ya kampeni kuhubiri amani.
Kwa upande wake mgombea ubunge jimbo la Bunda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Ester Bulaya, amesema katika kipindi hiki cha wiki mbili kilichobaki kuelekea uchaguzi mkuu lazima vyama vishikamane na kuwa makini sambamba na kulipongeza Jeshi la Polisi kwa kazi nzuri.
Mkuu wa
Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...