* Mwalimu Nyerere alizingatia Utawala Bora na kuichukia rushwa

Na Jovina Bujulu-MAELEZO


KILA ifikapo tarehe 14, mwezi Oktoba, Watanzania wanakumbuka kifo cha

muasisi wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambapo

mwaka huu atatimiza miaka 21 tangu afariki dunia.


Katika kipindi cha uongozi wake wa miaka 24, Taifa la Tanzania

limeshuhudia mafanikio lukuki katika nyanja za kilimo, viwanda, madini,

afya, elimu, maji na miundombinu. Mafanikio hayo bado tunayaona

yakiendelezwa na Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli.


Mwalimu Nyerere ni miongoni mwa viongozi ambao waliweza kukidhi

matarajio ya Watanzania kwa kuzingatia maadili ya uongozi na kujenga

umoja wa kitaifa katika watu wa makabila zaidi ya 120 wenye dini

tofauti,hivyo kudumisha amani ya katika Taifa la Tanzania kumepelekea Tanzania kuitwa “ Kisiwa cha Amani”.


Ni kiongozi aliyebeba historia ya Taifa la Tanzania kwa mawanda mapana

kwa sababu huwezi kuitaja Tanzania bila kumtaja Mwalimu Nyerere.

Wakati wa utawala wake alichukia rushwa na akapitisha sheria kwamba

mtu akila rushwa, aliyetoa na aliyepokea wote watapata msukosuko.


Katika kuzingatia maadili ya uongozi, Mwalimu Nyerere alichukia sana

rushwa na aliipiga vita kwa nguvu zake zote. Hali hii ilijionesha awali

wakati wa chama kilicholeta uhuru Tanganyika mwaka 1961 wakati huo

kikiitwa Chama cha TANU na baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM,)

ambapo katika mojawapo ya ahadi za chama cha TANU ilikuwa inasema,

‘Rushwa ni adui wa Haki, Sitatoa wala Sitapokea rushwa.’


Rushwa ni adui wa haki, na ni kitendo kibaya kwa hiyo watu wanaofanya

kitendo hicho ni wabaya sana na kitendo hicho hakifungamani na adili za

jamii ya Watanzania kwani kinamfanya mwenye haki kunyang’anywa haki

yake.

Kwa kuweka ahadi hii kuwa mojawapo ya ahadi za TANU inaonesha jinsi

Mwalimu Nyerere alivyokuwa amedhamiria kuondoa suala la rushwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...