MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)  Dk.John Magufuli akimnadi Askofu Josephat Gwajima 

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)  Dk.John Magufuli


Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)  Dk.John Magufuli amewapa pole wananchi wa Jimbo la Kawe kutokana na kuchelewa kwa maendeleo kutokana na kuwa na mbunge wa upinzani ambaye kwa kipindi cha miaka mitano ameshindwa kuwapigania na kuwatetea kimaendeleo.

Hivyo amewaaambia katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu wahakikishe wanamchagua mgombea ubunge wa CCM Askofu Joseph Gwajima ili ashirikiane naye kuleta maendeleo ya wananchi wa Kawe.

Akizungunza mbele ya wananchi wa Jimbo la Kawe na Kinondoni leo Oktoba 14 mwaka huu , Dk.Magufuli pamoja na mambo mengine ametumia nafasi hiyo kueleza anawapa  pole wananchi wa Kawe.

"Poleni Kawe,mmechelewa sana , miaka mitano nilikuja kuomba kura, na kwanafasi ya ubunge kulikuwa na mtoto wa Sinde Warioba, mimi mlinipa  lakini mbunge hamkunipa, nilileta maendeleo, nilitegemea mbunge wenu (Halima Mdee)atawatetea wana Kawe lakini hakufanya hivyo, hata nilipouliza mawaziri kama anawasumbua kukumbusha maendeleo ya Kawe nimaambiwa hasemi chochote.

"Hata hizi barabara ambazo tumejenga Kawe tumetumia nguvu kubwa sana.Mradi wa kuendeleza Jiji la Dar es Salaam DMDP  Kinondoni,Ilala,Temeke, Ukonga,Kigamboni wali pat miradi mingi lakini kwaa Kawe haikuwa hivyo kwasababu hakuna wa kuiomba.Mbunge wa  hapa Kawe akienda Bungeni anatoka nje na wakati mwingine anafunga mdomo sasa unaombaje miradi

"Nimekuwa Mbunge kwa miaka 20,nimekuwa Waziri kwa miaka 20, lazima mbunge ujenge mahusiano na mawaziri. Kawe haina hospitali ya kufanya operesheni, wakati Kigamboni wilaya mpya kuna hospitali mbili.Kawe hamjakosea Mungu ila mlikosea kuchagua, mwaka huu Kawe fanyeni mabadiliko,  nileteeni Gwajima tulete mabadiliko, najua kuna kampeni chafu zinaendekea za udini, na mitandaoni kuna fitina zinaendelea, leo hii wanasema Gwajima ni Askofu ,wanaingiza udini, 

"Mimimwenyewe nilitakiwa niwe Padri nikashindwa, aani nikae bila kuoa wakati mama Janeth yupo.Mimi ni Mkristo lakini jana nimeenda kuangalia maendeleo ya ujenzi wa Msikiti pale Kinondoni, ambao  niliuomba kwa Mfalme, wakati namuomba Mfalme huo msikiti alishangaa akaniuliza dini gani nikamwambia ni Mkristo.

"Kule Chamwino nimechangisha Wakristo kwa ajili ya kujenga msikiti mzuri wa kisasa tena wa ghorofa ambao utakuwa unaingiza waumini i 500, hiyo ndio Tanzania tuliyonayo na tuliyoachiwa na waasisi wa Taifa hili. Tanzania ambayo imeendelea watu wanaleta udini?

"Makabila yote yapo hapa mkutanoni na wakati leotunaadhimisha miaka 21 ya kukumbuka kifo cha .walimu Nyerere aliyepinga udini na ukabila halafu wanakuja watu wa kuanza kuleta udini,"amesema Dk.Magufuli wakati akimuombea kura Askofu Gwajima.

Amewaambia wananchi hao kwamba wakati akiwa Waziri ameshiriki kupima viwanja Kawe na kuongeza Kawe kubwa na wala haistahili kuwa hivyo ilivyo sasa.Hivyo amewaomba wampelekee Gwajima. "Nileteeni Gwajima, nileteeni Gwajima,mtaleta? Nina  machungu na Kawe,miaka mitano imepita sijafanya mambo makubwa Kawe, nataka kuleta maendeleo ya Kawe, katika miaka mitano ya urais wangu naomba mniletee Gwajima.

"Na baada ya Gwajima kuchaguliwa  kaa na watu hawa ili uwasikilize shida zao, ukae na akina mama na walemavu wapate mikopo inayotolewa na serikali, wapiganie wananchi masikini.Kuna eneo la bandari ya Mbweni ,kwani bandari nayo ni kero, watu kufanyabiashara pale ni dhambi, yaani wa Mbagala aende bandari ya Dar es Salaam halafu wa Kawe washindwe. Tena ngoja wakuchague ile bandari nitakupa na fedha za kuiendeleza.

"Sitaki kusema uongo,mbele ya viongozi wa dini,nataka siku nikifa nikafagie hata chumba cha Malaika, naomba mniletee.Gwajima hakuongoza , aliyeongoza ni mtoto wa dada angu anaitwa Furaha, dada yangu Asteria, kama kumleta ningemleta mtoto wa dada yangu.Akatae kama Furaha sio mtoto wa dada yangu.

"Wa pili Kiiziga ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Masharili, sio kwamba  hawafai lakini Gwagima amewazidi.Kazi ya ubunge inahitaji mtu jasiri,asiyeogopa, ana hofu ya Mungu, Kamati Kuu imeona Gwajima ndio anafaa kuwa Mbunge wa Kawe.

"Wangapi wataniletea Gwajima? , nileteeni Gwajima,Kawe hakuna viwanda vingi,mnadhambi gani, mmmebaki na kiwanda cha Wazo tu, tuna mipango ya kujenga viwanda kwanini kusiwe na viwanda Kawe, nipeni Gwajima tujenge viwanda,"amesema Dk.Magufuli.

Kwa upande wa Kinondoni, Dk.Magufuli amewaba wananchi wa jimbo hilo kuhakikisha wanamchagu mgombea ubunge Abass Tarima kwani anamfahamu vizuri na maisha yake yamekuwa Kinondoni."Nafahamu kuna changamoto ya mafuriko Kiinondoni ,tumepanga kutatua kero hiyo kwa kuujenga mto ng'ombe, hata hivyo baadhi ya mafuriko yanatokana na wananchi wenyewe."

Akimzungumzia zaidi  Dk.Magufuli amewapa siri Tarimba alifiwa na watoto wake wawili ambao alikuwa anawategemea ,mmoja ruban na mwingine injinia na wote walikufa ndani ya wiki moja."Nlipoenda kumpa pole na siku hiyo bado alikuwa anazubgumzia maendeleo ya Kinondoni, na nilimwambia nitatamani siku moja kama atagombea ubunge,Mungu akasikia na Tarimba akaongoza kura za maoni.

"Kama Kinondoni mnataka kulete mabadiliko ya kweli naomba mniletee Tarimba, ni mtu wa pekee.Hata hivyo wagombea  wetu kila mmoja anahistoria yake.Mgombea ubunge Ukonga Jeru Silaa baba yake alikufa wakati ananifanyia kampeni mwaka 2015, kijana wa watu alitulia, mwaka 2015 alikosa lakini tumemleta tena Ukonga naomba mniletee Jery silaa.Kila mgombea ana sifa yake hapa,"amefafanua Dk.Magufuli.

Mbali ya kuwazungumzia wagombea hao,Dk.Magufuli.amewaomba wananchi kuendelea kuwa wamoja na kuwataka wajiepishe na wagombea ambao wanachochea vurugu kwani mgombea urais mmoja wa tayari ameshakata tiketi ya ndege na uchaguzi ukishamalizika na kusababisha machafuko anaondoka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...