NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA VIJIJINI.
MGOMBEA
Ubunge Jimbo la Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani ,Michael Mwakamo
amewahakikishia wakazi jimboni hapo ,kushughulikia kero ya mifugo holela
ambayo hula mazao mashambani ambapo anaamini itabaki kuwa historia.
Aidha
amewataka wakulima kujiandaa katika kilimo na kwamba atahakikisha
anasimamia utekelezwaji wa sheria zilizopo, ili kupunguza tatizo hilo.
Mwakamo
ametoa kauli hiyo akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Ruvu kwa Dosa
Azizi, akiomba kura za kutosha kwa John Magufuli, Ubunge na Udiwani na
amewaomba wananchi hao kujitokeza kwa wingi Oktoba 28 kuwachagua
wana-CCM.
"Nakumbuka
miaka iliyopita mkulima alikuwa analima mpunga, akivuna anapanda
mahindi, miwa, maboga sanjali na mboga aina mbalimbali, ambapo kwa miaka
ya hivi sasa jambo hilo halipo, sitotumia nguvu nitakwenda kupambana na
wanaotakiwa kusimamia sheria zilizopo," alisema Mwakamo .
Awali
wazee wa Kijiji hicho wakiongozwa na Hemed Luwayo na Nuru Mshana
waliwafanyia matambiko ya kimira Mwakamo na mgombea udiwani Mwafulilwa,
yaliyolenga kuwaombea dua katika safari yao hiyo, ili wachaguliwe .
"Binafsi
najisikia vibaya leo hii ninapowaona wazee wetu wakiangaika katika
kujitafutia ridhiki kupitia kilimo, ambacho kwa miaka hii imekuwa
mtihani mkubwa unaosababishwa na ndugu zetu wafugaji wanaovamia maeneo
na mashamba," alisema Mwakamo.
Kwa
upande wake mgeni rasmi katika mkutano huo kutoka mkoani Rugemalira
Rutatina aliwataka wana-Ruvu kwa Dosa kuachana na ushabiki wa kisiasa,
badala yake wakichague Chama Cha Mapinduzi chini ya Mgombea wa Urais
Dkt. John Magufuli .
Mgombea
udiwani Kata ya Mtambani ,Godfrey Mwafulilwa alieleza,katika kijiji cha
Ruvu kwa Dosa miaka mitano iliyopita kilikuwa na changamoto ya
kukosekana kwa umeme na maji changamoto ambazo zimeshafanyiwa kazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...